Showing posts with label Karatu. Show all posts
Showing posts with label Karatu. Show all posts

Tuesday, April 23, 2013

Nimepata Ugeni Leo

Leo nilitembelewa na wageni ambao naonekana nao katika picha hii kushoto. Kuanzia kushoto ni Mzee Teri, Mrs Teri, mimi, Profesa Ann Wagner, Bill Green.

Bill Green, m-Marekani Mweusi kutoka South Central Los Angeles, akuwa afisa mojawapo wa masuala ya wanafunzi hapa Chuoni St. Olaf, hadi mwaka jana. Ananifahamu vizuri kutokana na miaka mingi tuliyofanya kazi pamoja hapa St. Olaf, na anafahamu shughuli zangu za kuwasaidia wa-Marekani wanaoenda Afrika.

Ni Bill Green ndiye aliyeandaa mpango wa mkutano wa leo. Aliniletea ujumbe wiki chache zilizopita kwamba ana watu ambao wanahusika na Tanzania na angependa kuwaleta Chuoni St. Olaf tuweze kuongea.

Tulivyokutana tu leo, Mzee na Mama Teri wamenikumbusha kuwa niliwahi kutembelea na kutoka mhadhara katika kanisa lao la Hossana, mjini Lakeville. Wana nakala ya vitabu vyangu: Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Matengo Folktales. Nami nimekumbuka kuwa ni kweli niliwahi kwenda kwenye kanisa hilo, kuchangia maandalizi ya waumini waliokuwa njiani kwenda Tanzania. Mada yangu ilikuwa tofauti za tamaduni, na watu walijipatia vitabu vyangu siku hiyo.

Mzee Teri na Mama Teri wameshafika Tanzania mara nyingi. Wanaifahamu sana Karatu.Wanamfahamu na wanamheshimu Dr. Wilbroad Slaa. Profesa Ann Wagner alifundisha hapa St. Olaf hadi alipostaafu miaka karibu ishirini iliyopita

Maongezi yetu ya leo yalihusu Tanzania, hasa masuala ya elimu katika ulimwengu wa utandawazi wa leo. Hao wazee wanajishughulisha na masuala ya kuchangia Tanzania. Leo tuliongelea zaidi elimu. Tulitathmini elimu  ipi ni sahihi kwa vijana wa Tanzania: wasome Tanzania au wasome nje ya nchi, kama vile Marekani? Faida au hasara zake ni zipi?

Monday, March 11, 2013

Maktaba ya Karatu

Wadau wa blogu yangu hii watakuwa wanajua jinsi ninavyoleta taarifa za maktaba mbali mbali, hasa zile ninazopata fursa ya kuzitembelea. Mfano ni taarifa hii hapa.

Mwaka huu, tarehe 7 Januari, nilipata fursa ya kuiona maktaba ya Karatu. Nilikuwa njiani kuelekea kwenye uwanja wa mnada, lakini papo hapo nilitaka kuiona maktaba. Kuna kibao nilikiona wakati natembea, kikielekeza iliko maktaba.

Nilipofika hapo nilipiga tu hii picha, nikaendelea na safari yangu ya mnadani. Maktaba iko juu kwenye sehemu ya mwinuko ambao nadhani ndio juu kabisa pale Karatu. Sikuingia ndani. Nikifika tena Karatu, nitaweka kipaumbele kuingia humo na kuona ilivyo. 


Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...