Wadau wa blogu yangu hii watakuwa wanajua jinsi ninavyoleta taarifa za maktaba mbali mbali, hasa zile ninazopata fursa ya kuzitembelea. Mfano ni taarifa hii hapa.
Mwaka huu, tarehe 7 Januari, nilipata fursa ya kuiona maktaba ya Karatu. Nilikuwa njiani kuelekea kwenye uwanja wa mnada, lakini papo hapo nilitaka kuiona maktaba. Kuna kibao nilikiona wakati natembea, kikielekeza iliko maktaba.
Nilipofika hapo nilipiga tu hii picha, nikaendelea na safari yangu ya mnadani. Maktaba iko juu kwenye sehemu ya mwinuko ambao nadhani ndio juu kabisa pale Karatu. Sikuingia ndani. Nikifika tena Karatu, nitaweka kipaumbele kuingia humo na kuona ilivyo.
No comments:
Post a Comment