Thursday, December 21, 2023

"Chickens in the Bus" Kusomwa Shuleni Cameroon

Leo, tarehe 21 Desemba, 2023, nimepata habari ya pekee kuhusu kitabu cha Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Mama mmoja kutoka Cameroon aishiye hapa Minnesota, na ni mmoja wa wale ambao wamafahamu kazi zangu miezi ya karibuni, ameniambia kuwa anahitaji nakala za Chickens in the Bus kwa ajili ya kuzipeleka kwenye shule Cameroon, ambayo yeye mi mmoja wa wahusika. Amesema wanahitaji nakala 20 ili kila darasa liwe na angalau nakala tatu. 

Taarifa hii imenifanya nirudie kukipitia kwa uangalifu kitabu hiki, nijiridhishe hakina kosa lolote. Naogopa kuwapa watoto wa shule kitabu chenye kosa. Kwa mtazamo wangu, kusambaza kitabu chenye makosa ni uhalifu. Kuwapa watoto kitabu cha namna hiyo ni kosa la jinai.

Saturday, October 7, 2023

KIKAO MJINI MAPLE GROVE, MINNESOTA


Tarehe 30 Septemba, 2023, nilikwenda Maple Grove, Minnesota, kuongelea kitabu changu cha Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Kikao kilifanyika katika maktaba ya Maple Grove. Tulitambulishana na wale ambao hatukufahamiana. Tulibadilishana uzoefu na mawazo. 

Aliyeandaa na kuendesha kikako ni Samba Fall wa Senegal aonekanaye kulia kabisa kwenye hii picha. Yeye ni mratibu wa Multicultural Kids Network pia mjumbe katika Hennepin County Race Equity Advisory Council. Yeye na mimi tumefahaiana kwa miaka kadhaa.

Wadau walipata fursa ya kununua vitabu vyangu. Hii itachangia tafakari na maongezi yetu kuwa endelevu. Papo hapa, ndugu Samba Fall anataka vikao vya aina hii vifanyika katika maktaba zote za Hennepin County. Tumekubaliana hivyo.




Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...