Hatukwenda mbali, tukaona duka la vitabu na moja kwa moja tukaingia humo.
Nilipoingia tu, kwenye meza moja karibu na mlango niliona ujumbe uliowekwa kwenye fremu, kuhusu vitabu. Nilivutiwa sana na ujumbe ulioandikwa na Clarence Day, Jr.
Nilimwuliza mama mhudumu humo dukani kama naweza kupiga picha. Alisema kwa uchangamfu kuwa ni sawa kabisa.
Jioni hii, wakati naandika habari hii kwenye blogu, nimetafuta taarifa nikagundua kuwa Clarence Day, Jr. aliandika ujumbe wake mwaka 1920. Kwa jinsi nilivyoupenda, nimeona niuweke hapa na nijaribu kuutafsiri kwa ki-Swahili. :
VITABU
Ulimwengu wa vitabu ni kitu kilichotukuka kwa namna ya pekee kilicholetwa na binadamu. Hakuna anachounda binadamu ambacho kinadumu hivyo: majengo ya kumbukumbu huanguka, mataifa hutokomea, himaya za ustaarabu hupitwa na wakati na kutoweka duniani; kufuatia zama za giza, mataifa mapya hujenga himaya zingine. Lakini ulimwengu wa vitabu una majuzuu yanayodumu daima, yakiwa na upya na ubichi kama siku yalipoandikwa, na yanaendelea kuelezea mioyoni mwa wanadamu kuhusu yaliyojiri hata mioyoni mwa wanadamu waliokwishafariki karne za zamani.
2 comments:
Safi sana Bwana Mbele na karibu sana Duluth
Kili Culture Team
Asante kwa ujumbe wako. Nafurahi kujua kuhusu Kili Culture Team. Tuzidi kuwasiliana.
Post a Comment