Mchungaji Mwalilino, ambaye alihitimu shahada ya uzamifu Luther Seminary, tuko wote hapa Minnesota, ingawa miji mbali mbali. Mgeni wetu, ambaye alihitimu shahada ya uzamifu katika Chuo Kikuu cha Augustana, Ujerumani, ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa. Mimi mwenye blogu hii nilihitimu shahada ya uzamifu katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison. Mjadala wetu ulikuwa wa kiwango cha juu kitaaluma. Tumeongelea utafiti katika tamaduni na dini za jadi za wa-Afrika, lengo moja muhimu likiwa ni kutafakari namna ya kuziweka dhana na falsafa za jadi za ki-Afrika kwenye uwanja wa mijadala na uchambuzi katika dunia ya leo, tukizingatia kuwa wa-Afrika wa tangu zamani wana mchango ambao unastahili kutambuliwa na kutumiwa.
Saturday, June 2, 2012
Watafiti wa ki-Tanzania Tumekutana Ughaibuni
Mchungaji Mwalilino, ambaye alihitimu shahada ya uzamifu Luther Seminary, tuko wote hapa Minnesota, ingawa miji mbali mbali. Mgeni wetu, ambaye alihitimu shahada ya uzamifu katika Chuo Kikuu cha Augustana, Ujerumani, ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa. Mimi mwenye blogu hii nilihitimu shahada ya uzamifu katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison. Mjadala wetu ulikuwa wa kiwango cha juu kitaaluma. Tumeongelea utafiti katika tamaduni na dini za jadi za wa-Afrika, lengo moja muhimu likiwa ni kutafakari namna ya kuziweka dhana na falsafa za jadi za ki-Afrika kwenye uwanja wa mijadala na uchambuzi katika dunia ya leo, tukizingatia kuwa wa-Afrika wa tangu zamani wana mchango ambao unastahili kutambuliwa na kutumiwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
4 comments:
safi sana!!inapendeza kwa kweli.
Dada Yasinta, shukrani.
Ngoja nikupe mfano wa hili tatizo. Sisi wa-Katoliki tuna usemi, "mimi ni mzabibu." Sasa tujiulize, je m-Nyasa wa Lundu na m-Ngoni wa Mgazini wanaujua mzabibu? Kuna uwezekano au umuhimu wa kuwaeleza dhana husika kwa kutumia tamathali zilizomo katika lugha zao ili fundisho la dini lieleweke kwao na liwe na maana kabisa kufuatana na utamaduni wao?
mheshimiwa Profesa Mbele asante sana kwa mada hiyo na hapo umenikumbusha huo mti wa mzabibu ni kweli huyo mnyasa au mhaya mimi ninayeandika hapa huo mzabibu sijui kama mababu zetu huko kwa wahaya wanaujua lakini bado na sisi katika kufanya ibada zetu(matambiko)tulikuwa na miti mfano kama unataka kufanya tambiko ni lazima mbele ya nyumba yako ya ibada yaani"msonge"uweke mti unaoitwa "ORUBUGU/O" YAANI HUU MTIkaramayake ni kwamba unaweza kuutoa ngozi au gambalake na kufanya shuka la kulalia zaidi ya mara sita baada ya hapo ndio mambo mengine yanaendelea yaa huo tunauita mti wa KAZOBA KA NYAMHUNGA,YAANI MTI WA MUNGU MUUMBAJI
Ndugu Anonymous, shukrani kwa mchango wako, mfano hai kutoka katika utamaduni wa wa-Haya. Ni mfano mzuri kabisa.
Hili suala ni zito, nami niliwahi kushiriki katika kulifafanua kwenye mkutano fulani wa wa-Luteri, kama nilivyoelezea hapa.
Post a Comment