Sunday, August 3, 2014

Watoto Katika Tamasha la Afrifest 2014

Kati ya watu waliotembelea meza yangu jana kwenye tamasha la Afrifest, alikuwepo mto anayeonaka katika picha hapa kushoto.

Ninawapenda watoto, Kila nikipata fursa ya kutembelea darasa la watoto, napenda kuwasimulia hadithi na mambo mengine. Nimefanya hivyo sehemu mbali mbali hapa Marekani, kama vile Colorado, Minnesota, na Pennsylvania.

Mtoto huyu alifika hapa mezani pangu ghafla, wakati namalizia kutafuna vipande vya kuku, Nilikuwa nimesalimiana na wazazi wake, kama nakumbuka sawa sawa, nao walikuwa pemdeni wakiangalia vitabu. Binti yangu Zawadi alipoona naongea na mtoto, alifanya uamuzi wa haraka wa kupiga hii picha, hata kabla sijasafisha meza, kwani mtu huwezi kujua mtoto atakuwepo hapo dakika au sekunde ngapi.

Unapoongea na motto, unakuwa katika mtihani mzito, wa kujua sio tu mambo ya kumwambia, bali namna ya kuongea naye ili avutiwe na aendelee kukusikiliza. Unapaswa kumweleza mambo yanayomgusa.

Binafsi, nikishauliza jina na mtoto, napenda kujua kama yuko shuleni. Na kama jibu ni ndio, natumia fursa hii kumhimiza mtoto kufanya bidii shuleni. Namsisitizia kuwa mimi nilipokuwa mtoto nilifanya bidii shuleni, na leo ninafundisha.

Napenda pia kuwatania watoto hao, kwa kuwaambia,  kwamba baadaye waje wasome kwenye darasa langu, na kwamba wawaambie wazazi  kuwa darasa langu litawafaa sana. Huwa nawaambia pia kuwa mimi ni msimuliaji mzuri wa hadithi, na hiyo habari ilionekana kumvutia mtoto huyu. Mtoto huyu hakuwa na haraka ya kuachana nami. Nilijisikia vizuri.

Nawapongeza wazazi wanaowaleta watoto wao kwenye shughuli kama haya matamasha, ambapo wanapafa fursa ya kuona mambo mbali mbali na kupanua ufahamu wao wa dunia kwa kiwango chao. Ni msingi bora katika maisha yao.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...