Friday, December 16, 2016

Dunia Yetu ya Maigizo

Shakespeare alisema, tena na tena, kuwa dunia ni jukwaa la maigizo ambapo kila mtu hujitokeza na kuigiza nafasi yake na kisha hutoweka zake. Maelezo haya naona ni kianzio muafaka cha kutafakari mambo ya dunia yetu. Ili kuchangia tafakari hiyo, nanukuu Hamlet, tamthilia maarufu ya Shakespeare, kutoka onyesho la 2, sehemu ya 2, ambapo tunasikia maongezi baina ya Polonius na Hamlet:

   Pol. My lord, I have news to tell you.
   Ham. My lord, I have news to tell you: when Roscius was an actor in Rome--
   Pol. The actors are come hither, my lord.
   Ham. Buzz, buzz!
   Pol. Upon my honor--
   Ham. Then came each actor on his ass--
   Pol. The best actors in the world, either for tragedy, comedy, history, pastoral, pastoral-comical, historical pastoral, tragical-historical, tragical-comical-historical-pastoral; scene individable, or poem unlimited, Seneca cannot be too heavy, nor Plautus too light. For the law of writ and the liberty, these are the only men.

Tangu zamani, nimevutiwa na ufafanuzi wa Polonius wa aina za maigizo. Kwa upande moja, naona kama analeta dhihaka nyepesi au kejeli, ingawa siwezi kudai kuwa ninaweza kuthibitisha jambo hilo. Ila kwa kweli anasisimua akili yangu.

Katika taaluma ya fasihi, inaeleweka kuwa ni juu ya kila msomaji kutumia ufahamu wake kuchambua kazi ya fasihi. Ufahamu huo unaweza kujumlisha mambo mengi, kama vile ufahamu wa fasihi, falsafa, na saikolojia. Matokeo ya kuchambua kazi ya fasihi hayabashiriki, na kwa kuwa kila msomaji ana upeo tofauti wa ufahamu, ni wazi kuwa kila msomaji wa kazi ya fasisi ataielewa kwa mtazamo tofauti.

Ukiwauliza wasomaji mbali mbali maana ya kazi fulani ya fasihi, utegemee kusikia majibu na maelezo tofauti, isipokuwa kama hao wasomaji wanafanya ukasuku. Kwa bahati mbaya, ukasuku huu umeshamiri miongoni mwa wengi. Hata katika blogu hii ya hapakwetu, wanajitokeza watu wanaoulizia maana ya kazi ya sanaa. Wanategemea niwape uchambuzi, kwa imani kwamba fasihi ni kama dini, ambamo kuna imamu au padri mwenye majawabu ya masuali ya waumini.

Baada ya maelezo haya, narejea tena kwenye ujumbe wangu wangu wa awali hapo juu, pamoja na nukuu niliyoiweka kutoka katika tamthilia ya Hamlet. Ninaona ni changamoto na kichocheo murua cha fikra.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...