Sunday, August 16, 2020

Tundu Lissu, Serikali ya CCM, na Ushoga

Kwa kuzingatia kuwa kuna upotoshaji mwingi kuhusu msimamo wa Tundu Lissu juu ya ushoga, napenda kusema kuwa msimamo wake unafanana na msimamo wa serikali ya CCM kuhusu ushoga.

Katika mahojiano kwenye kipindi cha "Hard Talk," yaliyotumia lugha ya kiIngereza, ambacho waTanzania wengi hawakijui, Tundu Lissu aliulizwa msimamo atakaochukua kuhusu ushoga endapo atakuwa na mamlaka. Alijibu kuwa hatajishughulisha na kupekua nini kinaendelea vyumbani mwa watu. Alimaanisha ataheshimu haki ya "privacy." Ikumbukwe kuwa haki hiyo imo katika katiba ya Tanzania pia.

Kwa upande wa serikali, baada ya kushambuliwa sana kutoka ndani na nje ya nchi kufuatia kauli za Makonda, wizara ya mambo ya nje ilitoa ufafanuzi kwamba kauli za Makonda si msimamo wa serikali ya Tanzania.

Wizara ilisema kuwa Tanzania inaheshimu mikataba yote ya kimataifa iliyosaini juu ya haki za binadamu. Tamko hilo lilitosha kuzimisha mashambulizi. Nami nilitamka na bado ninatamka kuwa serikali ilifanya busara kutoa hilo tamko la jumla, bila kuingia katika "details." Niko tayari kuelezea kwa nini ninasema kuwa serikali ilifanya busara kutoa hilo tamko la jumla.

Jambo la msingi ni je, hiyo mikataba ya kimataifa juu ya haki za binadamu ni ipi? Ni wazi kuwa muhimu zaidi ya yote na msingi wa yote ni tangazo la kimataifa la haki za binadamu. Haki ipi inayohusika hapa? Ni ile ile aliyoitaja Tundu Lissu, yaani haki ya "privacy."

Msimamo wa Tundu Lissu kuhusu ushoga unafanana na msimamo wa serikali ya CCM. 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...