Wednesday, August 24, 2016

Sheria ya Vyama vya Siasa, Tanzania

                           TANGAZO LA SERIKALI NA. 215 la tarehe 12/10/2007

                                              SHERIA YA VYAMA VYA SIASA
                                                       (SURA YA 258)

                                                           -------------
                                                            KANUNI
                                          (Zimetungwa chini ya fungu la 22(b))

                                KANUNI ZA MAADILI YA VYAMA VYA SIASA ZA
                                                         MWAKA 2007

                                                 SEHEMU YA KWANZA
                                                         UTANGULIZI

1. Kanuni hizi zinaitwa kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa Mwaka 2007 na zitaanza kutumika mara tu baada ya kutangazwa katika Gazeti la Serikali.

2. Kanuni hizi, zitatumika Tanzania bara na vilevile Tanzania Zanzibar

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale muktadha utaelekeza vinginevyo- “chama cha siasa” maana yake ni chama cha siasa chenye usajili wa kudumu kwa mujibu wa Sheria.
“Msajili” maana yake ni Msajili wa Vyama vya Siasa aliyeteuliwa kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria pia itajumuisha Naibu Msajili na Msajili Msaidizi;
“Sheria” maana yake ni Sheria ya Vyama vya Siasa.

                                                 SEHEMU YA PILI
                                                 HAKI YA CHAMA

4.–(1) Kila chama cha siasa kitakuwa na haki zifuatazo-

(a) Kutoa elimu ya uraia na elimu ya uchaguzi kwa wananchi kwa kufuata sheria na kanuni za nchi;
(b) Kutoa maoni ya kisiasa kadri itakavyoona inafaa ili kutekeleza sera zake, kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar;
(c) Kujadili na kushindanisha sera zake na zile za chama cha siasa kingine kwa lengo la kutaka kukubalika na wananchi;
(d) Kuwa na uhuru wa kutafuta kuungwa mkono na wapiga kura; na
(e) Kila Chama cha siasa kitakuwa na haki ya kufanya mikutano ya kisiasa na maandamano kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa;
(2) Wakati wa uchaguzi wowote utakaoendeshwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi, kila chama cha siasa kitakuwa na haki na uhuru wa kushiriki na kushirikishwa na Tume ya Uchaguzi na au chombo chochote chenye mamlaka katika kufanya uchunguzi na kupata matokeo katika jambo au suala lolote linalohusu uchaguzi.

                                                     SEHEMU YA TATU
                                                    WAJIBU WA CHAMA

5.-(1) Kila Chama cha Siasa kitakuwa na wajibu wa kutunza maadili chini ya kanuni hizi kwa: -
(a) kukieleza kwa wanachama wake ili kuongeza uadilifu wa kisiasa ndani na nje ya chama cha siasa;
(b) kulaani, kuepukana kuchukua hatua zitakazofaa ili kuzuia au kuepusha vitendo vya vurugu, uvunjaji wa Amani au ukandamizaji wa aina yeyote ile;
(c) kutotumia vyombo vya dola kukandamiza na kutoa vitisho kwa chama cha siasa kingine kwa manufaa yake;
(d) kutotoa maneno yoyote au maandishi ambayo ni ya uongo na kuhusu mtu yeyote au chama cha siasa chochote;
(e) kufanya mkutano wa kisiasa na maandamano bila kufanya vurugu kwa mujibu wa sheria za nchi;
(f) kulaani na kupinga-
(i) vitendo vyenye kuashiria ukandamizaji;
(ii) matumizi ya lugha ya matusi
(iii) vitendo vya kibabe na vurugu
(iv) matumizi ya nguvu ili kujipatia umaarufu wa chama au sababu yeyote ile;
(f) Kuepuka kuteremsha bendera iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria, kuharibu kwa namna yeyote ile kitu chochote ambacho ni ishara au nembo inayotumiwa na chama kingine kama sehemu ya utambulisho wa chama hicho;
(g) Kuepuka kushawishi kwa kutoa rushwa kama kichocheo ili kupata upendeleo au heshima kwa nia ya kufanikisha malengo;
(h) Kuepuka kutumia mamlaka. Rsilimali za serikali, vyombo vya dola, au wadhifa wa kiserikali, kisiasa au ufadhili wa nje ama wa ndani kwa namna yeyote ile ili kukandamiza chama kingine.
(i) Kuepuka vitendo vya ubaguzi wa rika, kabila, jinsia, dini na mahali alipozaliwa mtu yeyote ikiwa ni jamii au asili Fulani kwa kufanikisha malengo ya siasa; na
(j) Kuheshimu maamuzi halali yaliyofanywa kwa pamoja na vyama vyote.
(2) Kwa kuzingatia Sheria, kila chama cha siasa kitakuwa na uhuru wa kushirikiana na chama cha siasa kingine kwa nia njema kwa ajili ya kupanga vikao, mikutano ya hadhara kwa pamoja au maandamano kwa wakati mmoja kama kwamba mambo hayo yamefanywa na chama cha siasa kimoja au bila kuvunja sheria za nchi.

                                                         SEHMU YA NNE
                                                     WAJIBU WA MSAJILI

6.-(1) ili kuhakikisha kwamba Kanuni hizi zinatekelezwa, Msajili atakuwa na wajibu wa-

(a) kusimamia maadili ya vyama vya siasa;
(b) kupoekea malalamiko yaliyowasilishw
a pande zote;
(c) kuzuia kitendo cha uvunjaji wa Kanuni za maadili kisiendelee na kukitaka chama au kumtaka kiongozi wa chama kujirekebisha; na
(d) kutoa onyo la maandishi kwa chama au kiongozi wa chama husika;
(2) Iwapo baada ya kutolewa onyo la kwanza kwa mujibu wa Kanuni (1)(d), chama cha siasa kitaendelea au kiongozi ataendelea kukiuka maadili hayo, Msajili atakemea hadharani ukiukwaji huo wa maadili.

7.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni ya 5, malalamiko dhidi ya uvunjwaji au ukiukwaji wa maadili yatapelekwa kwa maandishi kwa mtu yeyote kwa maandishi yakiwa yamesainiwa na mlalamikaji.

(2) Mara baada ya kupokea malalamiko, Msajili ataanza kufanya Uchunguzi dhidi ya chama cha siasa kinacholalamikiwa.


Imesainiwa na,                                                         EDWARD N. LOWASA
Dar es Salaam                                                                Waziri Mkuu
1 Oktoba, 2007

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...