Thursday, March 23, 2017

Mpiga Debe wa Vitabu Amenifuata

Jana niliandika katika blogu hii kuhusu programu inayowapeleka watu wa Nebraska Tanzania, ambao wanashauriwa kusoma Africans and Americans Embracing Cultural Differences. Nilikiri kuwa niliandika kama vile ninajipigia debe, lakini nilipendekeza utamaduni huo.

Ilikuwa kama nimeota, kwani leo nimepigiwa simu na kuletewa ujumbe na kampuni ya Readers Magnet inayojishughulisha na utangazaji wa vitabu. Mama aliyenipigia alisemaa kuwa wanakifahamu kitabu changu kutokana na taarifa za wasomaji katika mtandao wa Amazon. Wangependa kukijumlisha katika orodha ya vitabu wanavyovitangaza, akafafanua mipango yao, ikiwemo kuwakilisha katika maonesho ya vitabu ya Frankfurt.

Kwa kuwa maelezo yalikuwa mengi, nilimwuliza kama anaweza kuniletea kwa maandishi, akakubali. Ameniandikia ujumbe, ambao unaanza hivi:

Your book, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, was recommended to us by our Book Scouts. We believe and we have validated that your unique book has the potential and our goal for your book is to be recognized or acquired by specific decision makers like book store owners, librarians, and traditional publishers who have connections and contacts to help you reach out to your target audience and increase your returns. Your book is sure to capture a lot of attention this coming 2017 Frankfurt International Book Fair in Frankfurt, Germany dedicated for titles like yours and positively we will be able to give them the same impression as we have realized to entice investors for your book.

Baada ya kusoma na kutafakari maelezo yote, nimekubali kushiriki mpango huo. Katika mazungumzo ya simu, Sophia alivyoniulizia mikakati yangu ya kutangaza vitabu vyangu, nilimjibu kwa uwazi kuwa mimi ni mwalimu na mwandishi. Sina uzoefu wa biashara, wala mkakati maalum wa kutangaza vitabu vyangu, bali kwa ujumla vinatangazwa na wasomaji wenyewe katika maongezi yao, mawasiliano yao, mitandaoni, kama vile blogu, na kama alivyojionea hapo Amazon. Kutokana na kwamba sina mkakati wala uzoefu wa kibiashara, nimeona kuwa sina hasara kuipa kampuni hiyo wadhifa wa kutangaza kitabu changu. Zaidi ya kwamba sina cha kupoteza, nimevutiwa na maelezo ya faida za kufanya hivyo.

Nimejisikia vizuri kutokana na mawasiliano ya leo na Sophia. Alivyonieleza namna walivyokifahamu kitabu changu, na nikatambua kuwa wanakihitaji, nilijikuta nikimhoji na kumwekea vizingiti. Sikutaka kuweka hata chembe ya fununu kwamba ninahitaji huduma yao. Ni wazi kuwa kama mtu una kitu cha thamani, una uwezo wa kuonyesha kuwa unajiamini. Utamaduni wa kujiamini na kujithamini ni muhimu kwa mtu binafsi, kwa jamii, na kwa taifa. Ndio maana, bila kusita, nilimwambia Sophia kuwa aniletee ujumbe wa maandishi ili nitafakari.

Nimeelezea ujumbe huu hapa kwa kuwa ninaamini unaweza kuwa na manufaa kwa waandishi wengine. Vile vile, ni jadi yangu kuandika katika blogu hii mambo yanayotokana na uzoefu wangu na ninayojifunza kuhusu masuala ya vitabu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...