Thursday, March 2, 2017

Nimemsikiliza Angela Davis Leo

Leo hapa chuoni St. Olaf tumepata fursa ya kutembelewa na Angela Davis, profesa na mwanaharakati maarufu. Kwangu imekuwa siku ya kumbukumbu. Mara ya kwanza kumsikiliza Angela Davis ni siku alipotoa mhadhara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mwaka 1974, kama sikosei. Nilikuwa mwanafunzi na ninakumbuka jinsi mwanaharakati huyu mrefu mwenye Afro kubwa kichwani alivyotusisimua kwa hotuba yake katika ukumbi wa Nkrumah.

Leo ameongelea hali ya ulimwengu kwa kuzingatia majanga yanayotokana na mfumo wa ubepari na mikakati ya kukabiliana yao.  Hotuba yake hii hapa:
https://www.stolaf.edu/multimedia/play/?e=1816

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...