Friday, November 17, 2017

Tamasha la Vitabu Minneapolis, 18 Novemba

Kesho nitahudhuria tamasha na vitabu liitwalo Minnesota Black Author's Expo mjini Minneapolis. Waandishi yaapata 40 watashiriki. Nami nitapeleka vitabu vyangu.

Itakuwa ni siku yenye shughuli nyingi za kukutana na wasomaji wa vitabu na kuongelea vitabu na uandishi. Kila mwandishi atapata fursa ya kutoa hotuba fupi kwa wahudhuriaji.

Pia kutakuwa na warsha juu ya uandishi, kwa yeyote atakayependa kujifunza.

Hili ni tamasha la kwanza la aina yake, na limeleta msisimko mkubwa katika jimbo hili la Minnesota. Lilibuniwa na kuandaliwa na waandishi Jasmine Boudah, Tovias Bridgewater Sly, na De'Vonna Pittman.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...