Showing posts with label Katoliki. Show all posts
Showing posts with label Katoliki. Show all posts

Sunday, September 20, 2015

Nimerejea Kutoka Kanisani

Nimetoka kanisani kusali, na ninaona ni sawa tu kuandika habari hiyo hapa katika blogu yangu. Hii si mara ya kwanza kwangu kuandika habari ya namna hiyo.

Kwanza napenda kuwajulisha ndugu, marafiki na wote wanaofuatilia habari zangu, kwamba afya yangu imeendelea kuwa bora. Zaidi ya huu mkongojo ninaotembea nao, uonekanao pichani, hakuna dalili ya tatizo. Naendesha gari mwenyewe, hata umbali mrefu. Natembea na mkongojo kwa kuwa daktari anataka nitembee nao. Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu.

Kama ilivyo kawaida, katika ibada ya misa ya leo tumewaombea watu wote. Tumewakumbuka waumini wenzetu wanaosali makanisani, misikitini, na katika nyumba za ibada za dini zingine, tukiombea amani ulimwenguni. Wa-Katoliki hatujiombei wenyewe tu, bali wanadamu wote.

Kila Jumapili, tangu Baba Mtakatifu wa sasa, Papa Francis II, alipotoa waraka wake wa kichungaji, Laudato Si, tumekuwa tukisali sala yake ya kuiombea dunia:

A prayer for our earth

All-powerful God, you are present in the whole universe
and in the smallest of your creatures.
You embrace with your tenderness all that exists.
Pour out upon us the power of your love,
that we may protect life and beauty.
Fill us with peace, that we may live
as brothers and sisters, harming no one.
O God of the poor,
help us to rescue the abandoned and forgotten of this earth,
so precious in your eyes.
Bring healing to our lives,
that we may protect the world and not prey on it,
that we may sow beauty, not pollution and destruction.
Touch the hearts
of those who look only for gain
at the expense of the poor and the earth.
Teach us to discover the worth of each thing,
to be filled with awe and contemplation,
to recognize that we are profoundly united
with every creature
as we journey towards your infinite light.
We thank you for being with us each day.
Encourage us, we pray, in our struggle
for justice, love and peace.

Leo Papa Francis yuko upande huu wa dunia, ziarani Cuba, akiwa njiani kuja Marekani na kuhutubia bunge la Marekani na pia Umoja wa Mataifa. Kuna msisimko mioyoni mwa watu, wanapongojea kusikia mawaidha ya kiongozi huyu aliyejipambanua kwa kutetea wanyonge na uangalifu wa dunia hii ambayo ni msingi wa maisha yetu na ya viumbe vyote.

Wednesday, March 2, 2011

Orijino Komedi Wamtangaza Yesu



Kibao hiki cha Orijino Komedi kiliniacha hoi kabisa tangu nilipokiona mara ya kwanza. Mimi ni m-Katoliki. Kila ninapokiangalia kibao hiki, naishiwa nguvu, kwa jinsi Orijino Komedi wanavyoimba na kukatika. Ni balaa babu kubwa. Papo hapo wanawasilisha ujumbe kwa namna isiyosahaulika. Najikuta nikisema Mungu asifiwe kwa vipaji alivyowajalia Orijino Komedi.

Nashukuru kwamba miaka zaidi ya kumi iliyopita niliamua kuanza kumtafakari Yesu mimi mwenyewe. Ninaamini kwa dhati kuwa, kwa jinsi alivyokuwa karibu na watu na pia mpenda michapo, Yesu angeafiki jinsi Orijino Komedi wanavyotangaza neno lake kwa huo mtindo wao wa kuyaruka majoka.

Nawashukuru sana Orijino Komedi kwa kuleta neno la Yesu kwa namna hii ya kuvutia na kugusa moyo.

Sunday, February 13, 2011

Kitabu Kuhusu Mtume Muhammad

Kati ya vitabu ninavyosoma wakati huu ni Muhammad: A Biography of the Prophet, kilichoandikwa na Karen Armstrong. Ni kitabu murua kwa jinsi kinavyoelezea mazingira aliyoishi Mtume Muhammad na harakati alizopitia katika kutimiza majukumu yake kama Mtume.

Kitabu hiki kinagusa na kuelimisha sana sio tu kuhusu historia ya u-Islam, bali pia kuhusu upekee wa Mtume Muhammad, kama Karen Armstrong anavyosema:

If we could view Muhammad as we do any other important historical figure we would surely consider him to be one of the greatest geniuses the world has known
(uk.52). (Tafsiri yangu: Kama tungemtazama Muhammad kwa namna tunayowatazama watu wengine muhimu katika historia, ni wazi tungemtambua kama mmoja wa watu wenye vipaji vya ajabu kabisa ambao dunia imepata kuwafahamu).

Karen Armstrong ni maarufu kwa msimamo wake kuhusu u-Islam. Anaelezea sana historia ya zile anazoziita hisia potofu kuhusu u-Islam na zilivyoanza na kuenea. Lakini, pamoja na kutafiti na kuandika sana kuhusu u-Islam, Karen Armstrong ni mtafiti wa dini zingine pia, kama vile u-Kristu u-Juda, na u-Buddha. Ni mmoja wa watu wanaoongoza hapa duniani kwa umakini wa kuandika kuhusu dini.

Pamoja na kusoma kitabu cha Muhammad na kufuatilia maandishi mengine ya Karen Armstrong, na pamoja na kufuatilia mihadhara na mahojiano aliyotoa sehemu mbali mbali za dunia, nafuatilia pia maandishi na matamshi ya wengine kuhusu mchango wa Karen Armstrong. Nimebaini kuwa kuna malumbano kuhusu mchango wake, ambalo ni jambo la kutegemewa katika taaluma.

Kitabu cha Muhammad ni kizuri na muhimu sana. Nafurahi kukisoma, kwani kinanifungulia milango ya kuyafahamu maisha na mchango wa mtu ambaye ametoa mchango mkubwa sana duniani. Ni kitabu muhimu kwa yeyote mwenye nia ya kumwelewa Mtume Muhammad na kuuelewa u-Islam.

Karen Armstrong, ambaye alikuwa sista katika Kanisa Katoliki, ambalo ndilo dhehebu langu, anatuonyesha mfano mzuri, kwa kujibidisha katika kuzifahamu dini za wengine. Naamini kuwa iwapo sote tungefanya hivyo, kungekuwa na maelewano mazuri baina ya watu wa dini mbali mbali.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...