Showing posts with label sala. Show all posts
Showing posts with label sala. Show all posts

Sunday, September 20, 2015

Nimerejea Kutoka Kanisani

Nimetoka kanisani kusali, na ninaona ni sawa tu kuandika habari hiyo hapa katika blogu yangu. Hii si mara ya kwanza kwangu kuandika habari ya namna hiyo.

Kwanza napenda kuwajulisha ndugu, marafiki na wote wanaofuatilia habari zangu, kwamba afya yangu imeendelea kuwa bora. Zaidi ya huu mkongojo ninaotembea nao, uonekanao pichani, hakuna dalili ya tatizo. Naendesha gari mwenyewe, hata umbali mrefu. Natembea na mkongojo kwa kuwa daktari anataka nitembee nao. Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu.

Kama ilivyo kawaida, katika ibada ya misa ya leo tumewaombea watu wote. Tumewakumbuka waumini wenzetu wanaosali makanisani, misikitini, na katika nyumba za ibada za dini zingine, tukiombea amani ulimwenguni. Wa-Katoliki hatujiombei wenyewe tu, bali wanadamu wote.

Kila Jumapili, tangu Baba Mtakatifu wa sasa, Papa Francis II, alipotoa waraka wake wa kichungaji, Laudato Si, tumekuwa tukisali sala yake ya kuiombea dunia:

A prayer for our earth

All-powerful God, you are present in the whole universe
and in the smallest of your creatures.
You embrace with your tenderness all that exists.
Pour out upon us the power of your love,
that we may protect life and beauty.
Fill us with peace, that we may live
as brothers and sisters, harming no one.
O God of the poor,
help us to rescue the abandoned and forgotten of this earth,
so precious in your eyes.
Bring healing to our lives,
that we may protect the world and not prey on it,
that we may sow beauty, not pollution and destruction.
Touch the hearts
of those who look only for gain
at the expense of the poor and the earth.
Teach us to discover the worth of each thing,
to be filled with awe and contemplation,
to recognize that we are profoundly united
with every creature
as we journey towards your infinite light.
We thank you for being with us each day.
Encourage us, we pray, in our struggle
for justice, love and peace.

Leo Papa Francis yuko upande huu wa dunia, ziarani Cuba, akiwa njiani kuja Marekani na kuhutubia bunge la Marekani na pia Umoja wa Mataifa. Kuna msisimko mioyoni mwa watu, wanapongojea kusikia mawaidha ya kiongozi huyu aliyejipambanua kwa kutetea wanyonge na uangalifu wa dunia hii ambayo ni msingi wa maisha yetu na ya viumbe vyote.

Friday, June 12, 2015

Siku ya Mhadhara Chuo Kikuu Winona Inakaribia

Siku hazikawii. Zimebaki siku kumi na moja tu kufikia siku ya mhadhara wangu Chuo Kikuu cha Winona, utakaotokana na utafiti wangu juu ya falsafa zilizomo katika masimulizi ya jadi kama inavyodhihirika katika kitabu changu cha Matengo Folktales. Niliandika taarifa ya awali ya mhadhara huu katika blogu hii.

Leo nimeamka nikiwa nauwazia mhadhara huu kwa dhati. Nimejikuta nikijikumbusha mambo muhimu. Ninataka kwenda kutoa mhadhara madhubuti, wa kusisimua na kuelimisha. Hili huwa ni lengo langu kila ninapokubali mwaliko kama huu wa kwenda kutoa mhadhara popote.

Ninatambua wajibu wangu wa kuitendea haki taaluma. Ni wajibu wangu kama mtafiti na mwalimu kuitendea haki taaluma. Ni wajibu wangu kuwa mfano wa kuigwa na vijana wanaotafuta elimu, kama hao vijana watakaonisikiliza Chuoni Winona.

Ninatambua wajibu wangu wa kuwathibitishia wanaonialika kwamba hawakukosea kwa kunialika. Ninataka wasikilizaji wangu wakiri kuwa uamuzi wa kunialika ulikuwa sahihi. Sitaki wanaonialika na wanaonisikiliza niwaache wakisema kuwa afadhali wangemwalika mtu mwingine. Sitaki. Nataka wote wakiri kuwa mimi ndiye niliyefaa kutoa mhadhara ule. Wakiri kuwa mimi ndiye niliyefaa kujibu au kujadili masuali yao.

Ninatambua wajibu wangu mbele ya Mungu. Uhai wangu siku hadi siku, akili timamu, na vipaji alivyonipa Mungu ni dhamana kwa faida ya wanadamu. Ninapovitumia vipaji hivi ipasavyo, ninatimiza wajibu wangu kwa Mungu. Ninamtukuza Mungu. Ni furaha kwangu kutambua kwamba kutumia vipaji kwa namna hii ni kumtukuza Mungu, sawa na kusali.

Hayo ndiyo mawazo ambayo yamekuwa yakizunguka akilini mwangu tangu asubuhi. Ni aina ya mawazo yanayonisukuma nyakati kama hizi, ninapojiandaa kutekeleza mialiko. Ninapokubali mwaliko, ninafanya hivyo kwa dhati. Nikiona sitaweza kwa vigezo nilivyofafanua hapa juu, huwa nakiri tangu mwanzo ili wahusika wamtafute mtu mwingine, hata kama kwa kufanya hivyo ninajikosesha malipo yanayoendana na mwaliko.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...