Wednesday, November 16, 2011

Mhadhara wa Jana Ulivyofanikiwa

Mhadhara wangu wa jana kwenye shule ya Mazingira, Apple Valley, ulifanikiwa sana. Ni umbali wa dakika 45 kutoka hapa ninapoishi. Niliongea kuanzia saa tatu hadi saa sita.










Leo Mwalimu Carlson ameniandikia ujumbe huu:

I have described the day to many of our faculty.... That was one of the best classroom sessions I have ever been a part of...the kids were buzzing for the rest of the day. Thank you so much
.

Nitafsiri kwa ki-Swahili:

Nimewaeleza walimu wetu wengi shughuli za leo.... Ni kati ya madarasa bora kabisa ambayo nimewahi kushiriki....vijana wamesisimka wakiongelea siku nzima. Asante sana.


Nahitimisha kwa kusema kuwa nilishagundua tangu zamani kuwa kuwaneemesha wengine kwa kuwafundisha ninayoyafahamu ni kitu kinachonipa raha mimi mwenyewe. Nafurahi kuwatajirisha vijana kitaaluma na kimtazamo. Mara kwa mara nafanya shughuli hizi kwa kujitolea, lakini sipungukiwi. Ninaamini ule usemi kuwa kadiri unavyotoa ndivyo unavyopewa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...