Thursday, November 3, 2011

Mwanafunzi Albino Aacha Shule Akihofia Kuuawa

Kila kukicha, zinajitokeza habari za kutia aibu, kusikitisha, na kutisha zinazothibitisha kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu. Hapa ni habari mojawapo kutoka blogu ya Francis Godwin kuhusu mtoto albino. Taarifa hizi za uhayawani zinapojitokeza huwa najiuliza kama Tanzania ni nchi kweli, au imeshakuwa jehenam.

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


Mtoto Albino aliyeacha masomo akifanya mahojiano na waandishi wa habari

MWANAFUNZI wa darasa la pili shule ya msingi Bulongwa wilaya ya makete mkoani Iringa Emeliana Chaula (9)mwenye ulemavu wa ngozi (albino) ambeye pia ni yatima anayelelewa katika kituo cha watoto yatima cha ELCT Bulonga Wilayani Makete ameacha masomo yake kwa kuogopa kuuwawa.

Mwandishi wa mtandao huu kutoka Makete Cony Mpila anaripoti kuwa mkuu wa kituo hicho Dr. Mcheshi alisema mtoto huyo amesimama kwenda shuleni kutokana na vitendo vya kutishiwa usalama wake na baadhi ya watu kutokana na umbali wa kutoka kituo hicho na shuleni anakosoma Emeliana.
Dr. Mcheshi alisema kituo chao kimeshindwa kumlinda mtoto huyo kutokana na changamoto ya ukosefu wa mafuta ya kumpeleka shuleni mtoto huyo. Ili kumnusuru mtoto huyo kimaisha na kumuwezesha aendelee na masomo kituo kimeiandika barua katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Makete ingawa hakuna jitihada zozote zinazoendelea katika kumnusuru mtoto huyo kimaisha na kimasomo.
Dr huyo alieleza pia kituo chake kinakabiliwa na changamoto ya kuwalea watoto yatima wenye umri mdogo na kukosa msaada kutoka katika jamii na serikali pia.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...