Tuesday, November 13, 2012

Nimeenda Tena Chuo Cha Mazingira, Minnesota

Leo nilitembelea tena Chuo cha Mazingira, mjini Apple Valley. Kama alivyofanya mwaka hadi mwaka, Mwalimu Todd Carlson alinialika kwenda kuongea na wanafunzi wake kuhusu uwiano baina ya masimulizi ya jadi na mazingira. Mwalimu Todd Carlson, anaonekana pichani kushoto kabisa










Mwalimu Carlson huwaeleza wanafunzi kuhusu masimulizi ya jamii mbali mbali za asili, kama vile wa-Marekani Wekundu, wenyeji wa asili wa Australia, na pia wa-Khoisan wa pande za kusini mwa Afrika.

Anatumia pia kitabu changu cha Matengo Folktales. Kila ninapoenda kuongea na wanafunzi hao, nawakuta wamesoma angalau sehemu fulani muhimu za kitabu hicho.



 


Kutokana na maandalizi hayo anayofanya Mwalimu Carlson, mazungumzo yangu na wanafunzi pamoja na masuali yao huwa ya kiwango cha juu.


Kama ilivyokuwa safari zilizopita, sote tumefurahia ziara yangu ya leo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...