

Watu waliniambia tangu zamani kuwa kanisa hili lilijengwa na wahamiaji kutoka Czechoslovakia, na kwamba madirisha yake ya vioo (stained glass) yanavutia sana. Nilikuwa na hamu ya siku moja kwenda kusali hapo na pia kuangalia hayo madirisha. Mimi hupenda nyumba za ibada za dini mbali mbali kama nilivyoeleza hapa na hapa.
Jana, kwa vile nilikuwa mjini hapo, nilihakikisha nimepiga picha ya kanisa hilo, ingawaje ni kwa nje tu. Nilipata fursa ya kuona kuwa pembeni mwa kanisa kuna shule. Huu ni utamaduni wa kanisa Katoliki, kwamba panapojengwa kanisa, na huduma zingine ziwepo, hasa shule na hospitali. Nilivyoliangalia hilo kanisa na hiyo shule, nilikumbuka kijijini kwangu, kwani kule nako hali ni hiyo hiyo.
No comments:
Post a Comment