Monday, April 22, 2013

Bunge Modern Taarab Kuzindua Albamu ya "FUCK YOU!"

CHANZO: Mwandishi Wetu

Mke_wa_Rais_Mama_Salma_Kikwete_akimnadi_mgombea_CCM jimbo_la_Kigoma_Mjini_Peter_Serukamba_5-10-2010             Bungeni,Dadoma

KITENDO cha wabunge wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania kugeuza jengo hilo lenye heshma ndani ya nchi kuwa jukwaa la malumbano na kuporomoshea matusi ya nguoni imewafanya watanzania kutokuwa na heshma tena na wabunge wao.
Bunge hilo ni moja ya mihimiri mikubwa Tanzania  iliyopewa heshma ya kutunga sheria mbalimbali ya za nchi pamoja na kupanga maisha ya watanzania kwa mwaka mzima kutokana na bajeti za serikali.
Matusi ya wabunge hao ndiyo iliyosababisha wakakumbwa na kashfa na dharau kila mahali huku wakitugiwa mashahiri mbalimbali na kupewa majina mbalimbali ya ajabu.
Moja dhihaka na dharau walizojizolea kutoka kwa wapikura wao ni pamoja kutungiwa bendi mahiri ya taarabu inayoitwa BUNGE MODERN TAARAB bendi hii iliyoanza kutoa matangazo ya kufanya uzinduzi wake wa kwanza inawakaribisha mashabiki wote kwenye uzinduzi wa albamu yao mpya kabisa iliyobeba jina la 'FUCK YOU'!.
NYIMBO hizi ambazo zipo katika mtindo wa mipasho, zitazinduliwa hivi karibuni kwenye ukumbi mmoja huko Dodoma! Albamu hiyo ina nyimbo tano na watunzi kwenye mabano!
1 Mkuki Kwa Nguruwe---(Anna Makinda)
2 Mimba zisizotarajiwa (Livingstone Lusinde)
3 Naongea na Mbwa Siongei na mwenye Mbwa (Juma Nkamia)
4 Mkuki kwa Nguruwe remix (Job Ndugai)
5 Come on fuck you (Peter Serukamba)
Wahi uzinduzi na nunua nakala yako halisi!!!!
Mbali na bendi hiyo pia kuna filamu mahiri iliyochezwa na wasanii mahiri waliosafiri kwa pesa za wananchi hadi  jijini Dodoma na kurekodi filamu hiyo katika Ukimbi wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania huku ikiongozwa na msanii mkongwe na mahiri wa sanaa ya muziki nchini Joseph Mbilinyi maarufu kama Mr II ama Sugu. Filamu hii itajia kesho hapahapa habarimpya.com usikose, habarimpya.com pia inawaruhusu wasomaji wake kuchati huku wakisoma habari ndani website kwani haina ya haja ya kurudi Facebook kwa ajili ya kuchati.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...