milima. Hizi nyumba ziko mwanzoni mwa mji wa Namanga, kabla hujafika kwenye geti la mpaka baina ya Kenya na Tanzania.
Thursday, May 5, 2011
Mitaani Namanga, 2007
milima. Hizi nyumba ziko mwanzoni mwa mji wa Namanga, kabla hujafika kwenye geti la mpaka baina ya Kenya na Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
5 comments:
Hapa mahali sijui kwanini napaogopa hasa kwa kuwa kuna marafiki zangu wajanja tu huwa wakijituliza tu kinamna fulu kuibiwa!
Siku hizi sishauri marafiki zangu wang'aeng'ae macho hapo na nakataza kabisa wasibadilishie manoti pesa hapo.
Ila kwa kukusoma naona labda sio kila mtu atulizaye manyanga hapo wajanja humgeuza dili!
Mie na bahati sichani nywele kwahiyo watoto tundu karibu wote huwa washkaji kwa kudhania mie RASTA halafu fulu mtundu kumbe wapi!
Unanifanya nipafikirie tena kivingine hapo Prof.
Si haba Profesa,kufanya ziara kama hizo,katika mitaa ya Namanga kuwepo katika miji tofauti utaona tabia za watu tofauti kulingana na mazingira tofauti na jamii tofauti za watu.
Ingawa sija fika huko lakini nimepapenda Namanga hasa kwa hekaheka zake za utafutaji wa maisha,mara nyingi watu wa mipakani wana shughuli nyingi zikiwemo na za wizi kama alivyo ogopa ndugu yangu Kitururu
Ninaimani wewe hukupata mkasa huo wa kuibiwa.Tuko pamoja nawe daima.
Ndugu Kitururu na Mzee Sikapundwa, shukrani kwa mchango wenu. Nami napenda nichangie tena kidogo.
Mara ya kwanza kuiona Namanga ilikuwa mwaka 1989 nilipokuwa nakwenda Kenya. Upande wa Kenya kulikuwepo na jamaa wengi wanaobadilisha hela.
Lakini miaka hii ya karibuni, hakuna haja ya yote hayo, kwani ninatembea na kadi ya kuchukulia hela badala ya hela taslimu.
Mara ya kwanza nilipolala hapo Namanga niliona kuna ujirani mwema kweli baina ya wa-Kenya na wa-Tanzania. Ukiingia hoteli au baa za upande wa Tanzania, unawakuta wa-Kenya kibao, na wewe m-Tanzania unajivukia mpaka na kwenda kupata ulabu upande wa Kenya.
Wenyeji waliniambia kuwa kwa hapo hapo mpakani, huhitaji kibali kuingia nchi jirani. Kibali unahitaji unapoenda ndani zaidi ya nchi.
Mfanyabiashara wa kwanza niliyemfahamu hapo Namanga ni m-Chagga mmoja akiitwa Bwana Mangelepa. Alikuwa anamiliki Heshima Bar. Hii baa haiko tena, ila mwaka 1989 na 1990 nilikuwa nakata kiu hapo :-)
Ila Prof. hilo toto la Kimasai lililokuwekea mkono begani hukulipa lavu yani ! Limetoka kikujipendekeza kweli kwenye hiyo Picha Profesa Jay.
Kukiachana nahilo!
Kupitia njia hiyo ya NAMANGA mara yangu ya kwanza ni 1996 .Nampaka leo sijawahi kusumbuliwa hapo ila wadau niwajuao mpaka kwenye viofisi vya kubadili pesa pale washaliwa fweza yani!:-(
Ila nimesha farijiwa sana tu hapo kikukata kiu ingawa kuna mchezo naustukia ukionekana unakata kiu kiurahisirahisi unaanza kuletewa sana biashara kitalii hapo kitu kiwezacho kufanya uondoke umenunua bangili ambazo inabidi utunge umpe nani kama zawadi!:-(
Kaka usemayo ni kweli. Nimepita Namanga zaidi ya mara hamsini hivi. Ni pazuri sema kuna uwezekano pakawa mazalio mazuri ya ukimwi, ujambazi, biashara haramu, madawa ya kulewa hata kupitisha magaidi. Kitu cha kusikitisha ni ufisadi wa maafisa wa mpakani pale. Nilishuhudia mara nyingi wakiwanyanyasa na kuwatoa rushwa akina mama wafanyao vijibiashara za kuvusha vitu adimu. Pia kuna wasomali wengi wanaofanya biashara ya kubadili fedha kinamna.
Kwa ujumla Namanga ni pazuri hasa upande wa Tanzania ambapo kuna vivutio vingi kuliko upande wa Kenya. Namanga ni pazuri kuliko Holoholo ambako kuna umbali mrefu baina ya posts mpakani.
Post a Comment