Sunday, June 22, 2014

Ziara Fupi Mjini Northfield, Minnesota

Jana alasiri, binti yangu wa kwanza, Deta, alinipeleka hapo katikati ya mji, eneo la posta. Nilitaka kwenda kuangalia mafuriko ya mto Cannon, ambayo niliyaelezea jana katika blogu hii. Hapa naleta picha kadhaa alizopiga. Sikujua kama amewahi kupiga picha.









 
Nilifurahi nilipoziona picha alizopiga, ingawa yeye si mzoefu. Ninaonekana katika hizi picha zote. Katika picha mbili, mto wa Cannon, ambao umefurika, unaonekana pia.












Nimezileta picha hizi ili kuwathibitishia ndugu na marafiki kuwa hali ya afya yangu inaendelea kuwa njema, ingawa imechukua miezi mingi sasa. Ninategemea kuanza kufundisha tena wakati muhula mpya wa shule utakapoanza, wiki ya kwanza ya mwezi Septemba, Insha'Allah.










Hapa kushoto naonekana nimeketi sehemu ya "park" hapa mjini. Nimeshika mkongojo ambao umenisaidia kutembea kwa miezi kadhaa, ila sasa naweza kutembea bila kuutumia.Nimetoka mbali; namshukuru Mungu.

2 comments:

Anonymous said...

Pole sana Prof.

Mbele said...

Asante sana. Nilikuwa nimekongoroka kweli, ila sasa afadhali. Namshukuru Muumba.

Kila tunapoamka tukiwa wazima na afya nzuri, tushukuru, kwani sio haki yetu. Tutumie fursa hii kwa manufaa ya wanadamu. Ndilo jambo ambalo nimejifunza, baada ya afya kukongoroka kwa miezi, nikashindwa kufanya shughuli nilizozizoea, kama vile kusoma, kufundisha, na kuandika.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...