Tuesday, June 3, 2014

Wanafunzi Wangu Kwenye Lango la Ngorongoro

Katika mizunguko na wanafunzi wangu kaskazini mwa Tanzania, mwezi Januari 2013, tulifika pia kwenye hifadhi za Taifa.

Picha hii hapa kushoto nilipiga kwenye lango la kuingilia Ngorongoro. Tulikuwa tumeshaangalia ndani,  na sasa tulikuwa tunarudi tena kwenye magari, kuendelea na safari ya kuingia katika hifadhi.

Walikuwepo wanafunzi 29, wote kutoka chuo cha St. Olaf, Minnesota, ambapo nafundisha. Niliwaleta Tanzania kujifunza kuhusu mwandishi Ernest Hemingway: safari zake na kuishi kwake Afrika Mashariki, tukiwa tunasoma maandishi yake kuhusu sehemu hizo, hasa Green Hills of Africa na True at First Light, na pia hadithi fupi, barua, na makala katika majarida.

Hemingway alisafiri na kuishi Afrika Mashariki miaka ya 1933-34 na 1953-54.

Wanafunzi waliifurahia sana safari hii na walijifunza mengi, ambayo kwa ujumla huwa hayafundishwi katika vyuo. Nimefanya utafiti wa miaka karibu kumi, na ndio msingi wa kutunga kozi hii iitwayo "Hemingway in East Africa." Nimeandika mara kadhaa katika blogu zangu kuhusu kozi hii.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...