Miaka ya karibuni nimepata msisimko wa kuandika kwa ki-Swahili, ili kujitoa katika giza la ujinga linalotukabili wasomi wengi. Ujinga huu ni pamoja na kutoelewa namna ya kutumia ki-Swahili ipasavyo, na pia kudhani kuwa ki-Swahili hakina uwezo sawa na lugha zingine katika kuelezea mambo, hasa taaluma.
Ninajitahidi kujikomboa. Mwaka jana, kwa mfano, niliandika makala nyingi kwa ki-Swahili, hadi nikachapisha kitabu. Wakati wa kuandika nilisoma kazi kadhaa za Shaaban Robert ili kujijengea uwezo na kujiamini katika kutumia lugha ya ki-Swahili. Ni kama muujiza kuwa leo nimeletewa majarida haya, kwani kiu yangu ya kujielimisha bado na itaendelea kuwa kubwa.
Natoa shukrani tele kwa Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kunikumbuka hivyo.
3 comments:
Dah! Sijui hata niseme nini. Ni juzi tu hapa nilikuwa naulizia habari za jarida hili (na mengineyo) kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili pale Mlimani. Nitajaribu kulitafuta hata kama ikibidi kumwambia mkutubi wetu hapa anayeshughulikia Afrika kuanza kuliagiza jarida hili na lile la KISWAHILI kila yanapotoka. Nikupe hongera prof. kwa KUKUMBUKWA!
pia sikujua kama jarida la tabaruku ya maprofesa Besha na Mochiwa lilishatoka. Hawa walikuwa walimu wangu wapendwa na ningependa sana kutoa mchango wangu kuwakumbuka.
Hili toleo la tabaruku ya Profesa Besha na Mochiwa ni kati ya hayo niliyoletewa. Ni Juzuu namba 6, 2008.
Mimi nimo katika kamati ya uhariri, na ndio kisa cha kukumbukwa.
Nitaweza kukuletea angalau orodha ya makala zilizomo katika majarida haya.
Nategemea kwenda huko hivi karibuni na nitakwenda kuyakusanya haya majarida na vitabu vingine. Kila nikienda huko begi langu huwa linajaa vitabu wakati wa kurudi mpaka wakati mwingine huwa inabidi kulipia faini kwenye ndege kwani vitabu ni vizito sana.
Orodha ya makala zilizomo katika jarida la tabaruku za profesa Besha na Mochiwa tu zinatosha.
Asante mwalimu
Post a Comment