Sunday, April 10, 2011

Kuwalea Watoto Katika Usomaji Vitabu

Huwa natafakari sana suala la kuwalea watoto katika usomaji vitabu. Mtoto huyu hapa kushoto alikuwa anaangalia vitabu vyangu katika maonesho ya elimu na ajira yaliyofanyika mwaka jana Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam. Hiki kitabu alichoshika kinaitwa CHANGAMOTO.

Katika matamasha ya aina hiyo, hasa ya vitabu, navutiwa ninapowaona wazazi wamekuja na watoto wao. Huku Marekani ni jambo la kawaida.

Katika tamasha hilo la elimu na ajira Dar es Salaam, nilimwona mama mmoja amekuja na mtoto wake. Mama huyu, anayeonekana katika picha hii, alikuja kwenye kibanda changu, ambapo nilikuwa nimeweka vitabu vyangu, akaniuliza masuali kadhaa, huku mwanawe akisikiliza. Niliongelea masuali yake, kuhusu shughuli zangu katika elimu na uandishi, na kadhalika. Ilikuwa ni fursa kwangu pia ya kumhamasisha mtoto wake. Sitasahau mfano alioonyesha mama huyu. Wahenga walisema, mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.

Picha hii ilipigwa Minneapolis, Oktoba 4, 2008, wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya Uhuru wa Nigeria. Mama huyu m-Nigeria alikuja kwenye meza yangu ya vitabu na huyu mwanae. Tuliongea, wakaangalia vitabu vyangu na kuvinunua. Kutokana na mfano wa mzazi, mtoto anapata ufahamu kuwa vitabu ni muhimu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...