
Profesa Zust ameshawapeleka wanafunzi Tanzania mara kadhaa. Katika kuwaandaa, hutumia kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na pia hunialika nikaongee nao. Anajisikia vizuri sana ninapokutana na wanafunzi wake kujibu masuali yao na kuwapa maelezo mbali mbali, nami huwa nafurahi kukutana na wanafunzi hao wanaosomea taaluma ambayo sikusomea, ila ni wazi kuwa wanafaidika na mawazo yangu kuhusu jinsi tofauti za tamaduni zinavyohusika katika taaluma yao.
Wanafunzi hao na profesa wao wanapata fursa ya kuona sehemu mbali mbali za Tanzania, kama vile hospitali ya Ilula, kijiji cha Tungamalenga, na hifadhi ya Taifa ya Ruaha. Sehemu zote tatu ziko Iringa. Wanafunzi hao wanaguswa sana na ziara yao Tanzania. Nimeshasoma baadhi ya maoni yao.
Mwaliko wa sasa ni wa kuongea na wanafunzi tarehe 2 Januari. Insh'Allah, nitaleta picha na taarifa.
Mwaliko wa sasa ni wa kuongea na wanafunzi tarehe 2 Januari. Insh'Allah, nitaleta picha na taarifa.
No comments:
Post a Comment