
CCM ina kila sababu ya kujivunia vijana wake, yaani UVCCM. Sio tu ni vijana wanaozingatia wajibu wao wa kutetea na kutekeleza ajenda za serikali ya CCM, kama wanavyotamka
katika tovuti yao, bali ni wakakamavu, ambao wako tayari kwa lolote.
Hapa naleta picha kadhaa kuthibitisha jambo hilo, nikizingatia usemi wa ki-Ingereza kwamba "a picture is worth a thousand words," yaani picha ina thamani sawa na maneno elfu. Jionee mwenyewe uwajibikaji na utendaji wa hao vijana.

Kwenye masuala ya itikadi, vijana hao wako mstari wa mbele pia. Angalia hilo bango walilobeba katika maandamano yao huko Visiwani.
Kama hizi picha hazitoshi kukushawishi, basi angalia video hii hapa chini. Kwa kweli, CCM ina kila sababu ya kujivunia vijana wake.
No comments:
Post a Comment