Monday, September 3, 2012

Nimekutana na Wanablogu Songea


Mwaka huu, kwa mara nyingine, nilifanikiwa kufika Songea, nikaonana na Ndugu Christian Sikapundwa, mmiliki na mwendeshaji wa blogu ya Tujifunze Kusini. Hii ilikuwa ni mara pili kukutana, kwani tulishakutana mwaka jana pia, kama nilivyoripoti hapa. Tulifurahi kukutana tena, tukabadilishana mawazo na kupiga michapo kuhusu mambo mbalimbali. Kwa vile sisi wote ni walim, tulikuwa na mengi ya kuongelea. Hapa kushoto tunaonekana tukijipongeza na kushukuru kwa kukutana.






Hapa kushoto tunaonekana tukiwa na mdogo wangu na binti yake.













Katika pita pita yangu kwenye eneo la Chuo Kikuu kipya cha Mtakatifu Augustin (SAUT),  tarehe 21 Julai, nilikutana na jamaa ambaye alijitambulisha kuwa ni Willy Migodela, mmiliki na mwendeshaji wa blogu ya mtandao-net. Nilifurahi kukutana naye, kwani mimi ni mmoja wa wadau wa blogu yake. Ni yeye aliyenitambua tulipoonana. Alisema kuwa alikuwa mwanafunzi katika darasa la uzamili la Profesa Mugyabuso Mulokozi, ambamo niliwahi kutoa mhadhara, kama nilivoelezea hapa. Wanafunzi wengine wa darasa lile wameshajitokeza kwangu na kujitambulisha, nami nafurahi sana.

Ndugu Migodela kwa sasa anafundisha chuoni SAUT. Nilikitembelea chuo hicho siku hiyo na Siku chache zijazo, Insh'Allah, nitaandika taarifa za ziara yangu hapo chuoni.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...