Monday, September 24, 2012

Tamasha la Vitabu "Twin Cities" Linakaribia

Tamasha la vitabu liitwalo Twin Cities Book Festival litafanyika tarehe 13 Oktoba mjini St. Paul, Minnesota. Litafanyika kwenye sehemu maarufu iitwayo State Fairgrounds. Hii ni mara ya kwanza kwa tamasha hili kufanyika nje ya mji jirani wa Minneapolis. Nimeshiriki tamasha hili kwa miaka kadhaa, kama nilivyoelezea hapa na hapa.

Mimi kama mwandishi wa vitabu nimeshalipia meza. Hapa pichani ni vitabu vyangu nitakavyopeleka kwenye tamasha. Sasa nangojea tu siku ije, nikajumuike na wadau mbali mbali katika nyanja za uandishi, uchapishaji, uuzaji, na uchambuzi wa vitabu.  Nangojea kuwashuhudia tena maelfu ya watu wa hapa wakiwa katika heka heka za kuangalia vitabu, kuvinunua, kuongea na waandishi, wachapishaji, wauza vitabu, na kadhalika.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...