Wednesday, April 29, 2015

Maelezo Zaidi Kuhusu Filamu ya "Papa's Shadow"

Wakati huu ninapoandika makala hii niko na binti zangu Deta na Zawadi, tunaangalia filamu ya Papa's Shadow, iliyotngenezwa na Jimmy Gildea, aliyekuwa mwanafunzi katika kozi niliyofundisha Tanzania Januari, 2013. Nimeshaitaja filamu hii katika blogu hii

Maelezo yanayoambatana na filamu ni haya:

FEATURING AN EXCLUSIVE TESTIMONY GRANTED BY HIS SON, PATRICK HEMINGWAY, PAPA'S SHADOW DIVES HEAD FIRST INTO AUTHOR ERNEST HEMINGWAY'S HUNTING EXPEDITIONS IN EAST AFRICA AND THEIR DEFINING ROLE IN SHAPING A LEGEND.

YOUNG FILMMAKER JIMMY GILDEA DOCUMENTS HIS EXPERIENCE WHILE STUDYING HEMINGWAY UNDER THE INSTRUCTION OF AFRICAN AUTHOR JOSEPH MBELE, JOURNEYING ACROSS MIDWEST AMERICA, THROUGH THE SERENGETI PLAIN AND UP THE STEEP CLIFFS OF MT. KILIMANJARO.

HEMINGWAY'S SON PATRICK AND MBELE ENGAGE IN AN INSPIRATIONAL AND REVEALING CONVERSATION REGARDING THE FAMOUS AUTHOR'S FASCINATING RELATIONSHIP WITH EAST AFRICA.

THIS PERSONAL AND EMOTIONAL FILM EXPOSES MANY ANSWERS TO QUESTIONS HEMINGWAY FANS HAVE ALL BEEN WAITING FOR.

Hii ni mara yangu ya pili kuiangalia filamu hii, na kuona jinsi Mzee Patrick Hemingway na mimi tunavyomwongelea Ernest Hemingway: maisha yake, uandishi wake, na falsafa yake. Ninajionea faida ya kusoma, kusoma kwa dhati, bila kuchoka. Ninafurahi kuwa wanangu wanajifunza jambo kutoka kwangu.

Lengo langu kuu katika kuunda kozi yangu, ambayo ni chimbuko la filamu hii, lilikuwa kuuelimisha ulimwengu kuhusu namna Hemingway alivyoipenda Afrika Mashariki. Kwa upande wa Tanzania, nilitaka walimwengu wafahamu namna Hemingway alivyoandika kuhusu Serengeti, Mlima Kilimanjaro, na kadhalika. Huu ni ukweli juu ya Hemingway ambao haufahamiki vizuri, au umefunikwa kwa makusudi kwani wengi, wamezoea tangu zamani kuiona Afrika kwa dharau. Filamu hii itasaidia kurekebisha jadi hiyo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...