Hata hivi, napenda niseme kuwa siku kadhaa kabla ya tamasha, nilipomwambia mratibu kuwa mwaka huu ninayo bendera ya Tanzania, aliniambia kuwa tayari wamenunua. Nilipatwa na mshangao wenye furaha.
Kuna nchi nyingi duniani, na nchi zilizotarajiwa kuwakilishwa na bendera ni ishirini na kidogo. Sikupata wasaa wa kuulizia walifikiaje uamuzi wa kununua bendera ya Tanzania. Ninahisi ni kwa sababu nilikuwa nimejisajili kama mshiriki wa tamasha, na pia kwa kuwa nina historia ndefu ya kushiriki matamasha mjini Faribault na majukumu mengine mjini Faribault.
Nilielezea kifupi Tanzania iko wapi na historia yake. Nilielezea maana ya rangi za bendera ya Tanzania, kasha nikaimba wimbo wa Taifa. Naamini kuwa hii ni mara ya kwanza kwa wimbo wa Taifa wa Tanzania kusikika mbele ya kadamnasi mjini Faribault. Nitakumbuka tukio hili.
Sehemu kubwa ya filamu hiyo ni maongezi baina yangu na Mzee Patrick Hemingway kuhusu maisha, uandishi, na falsafa ya baba yake, mwandishi Ernest Hemingway.
Tamasha limefana sana. Nimekutana na kuongea na watu wa mataifa mbali mbali. Nimepanua mtazamo na ufahamu wangu kwa kuwasikiliza, na mimi nimewafahamisha mambo kadha wa kadha ambayo walikuwa hawayajui.
Kama nilivyogusia, hapa nimeweka picha mbali mbali, bali nategemea kuandika taarifa na kumbukumbu siku zijazo.
No comments:
Post a Comment