Tumesafiri na wadau wa programu ya Bega kwa Bega, ambao wanaishi Minnesota. Hii ni programu inayowashirikisha wa-Marekani na watu wa Iringa katika mipango mbali mbali ya maendeleo, kama vile elimu, afya, na maji safi. Ingawa mimi sikuwafahamu wadau tuliosafiri nao leo, wote wananifahamu. Wameniambia kuwa mwaandaaji na kiongozi wa safari yao, ambaye anaonekana pichani, wa pili kutoka kulia, aliwahimiza kusoma kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Ni faraja kwa mwandishi yeyote kujua kuwa watu wanasoma maandishi yake.
Tumefikia Iringa Lutheran Centre, na tutakuwa hapa wiki moja. Wadau wa hapa tunaweza kuonana katika siku hizo. Namba zangu za simu ni 0754 888 647 na 0717 413 073
No comments:
Post a Comment