Tuesday, August 9, 2011

Nimeingia Iringa Jioni Hii

Jioni hii nimeingia mjini Iringa, nikitokea Dar es Salaam. Nimekuja na wanafunzi katika programu ya LCCT ambayo huleta wanafunzi kutoka vyuo vinne vya Marekani kuja kusoma chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa muhula moja, na pia huwawezesha wanataaluma na maafisa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenda kwenye vyuo hivyo kwa utafiti au kujiongezea uzoefu kwa miezi minne.

Tumesafiri na wadau wa programu ya Bega kwa Bega, ambao wanaishi Minnesota. Hii ni programu inayowashirikisha wa-Marekani na watu wa Iringa katika mipango mbali mbali ya maendeleo, kama vile elimu, afya, na maji safi. Ingawa mimi sikuwafahamu wadau tuliosafiri nao leo, wote wananifahamu. Wameniambia kuwa mwaandaaji na kiongozi wa safari yao, ambaye anaonekana pichani, wa pili kutoka kulia, aliwahimiza kusoma kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Ni faraja kwa mwandishi yeyote kujua kuwa watu wanasoma maandishi yake.

Tumefikia Iringa Lutheran Centre, na tutakuwa hapa wiki moja. Wadau wa hapa tunaweza kuonana katika siku hizo. Namba zangu za simu ni 0754 888 647 na 0717 413 073

Picha zinazoonekana hapa tumepiga tukiwa katika hoteli mmoja Mikumi, tuliposimama ili kupata chakula cha mchana.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...