Tuesday, August 30, 2011

Safari ya Bagamoyo

Mizunguko yetu nchini Tanzania imemalizika. Safari yetu ya mwisho tulienda Bagamoyo, tarehe 27 Agosti. Tulitembelea Caravan Serai, ambayo ni makumbusho ya historia. Nilitaka wanafunzi wangu wapate fununu kidogo ya umaarufu wa Bagamoyo katika historia.







Historia hii imejumlisha mambo mengi, ikiwemo biashara ya watumwa na pembe za ndovu, mji huu kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni ya wa-Jerumani, mapigano ya Bushiri dhidi ya wa-Jerumani. Kwa upande wangu kama mwanafasihi, naukumbuka mji wa Bagamoyo kwa vile hapo aliishi Mgeni bin Faqihi, mtunzi wa "Utenzi wa Rasi 'lGhuli," ambao ni hazina kubwa katika urithi wa utamaduni wetu, ingawa wengi hawaujui. Labda iko siku jamii yetu itaamka.

Tulizunguka mitaani, hadi ufukweni, tukafaidi upepo mwanana na mandhari ya kuvutia. Kwa hayo na mengine mengi, Bagamoyo ni mji maarufu kwa utalii.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...