Friday, September 9, 2011

Hoteli ya Masista, Mbamba Bay

Mwaka huu nilipotembelea Mbamba Bay, tarehe 2 hadi 4 Agosti, nilifikia katika hoteli ya St. Bernadetha ambayo ni ya masista wa Kanisa Katoliki. Ni mradi wao katika kuendeleza huduma kwa jamii. Papo hapo, kuwepo kwa hoteli hii ni kivutio kwa utalii.

Ukiwa mjini Mbamba Bay, hoteli hii inaonekana vizuri, kwani iko kilimani. Ukiwa hapo hotelini, unaliona Ziwa Nyasa vizuri na mji wa Mbamba Bay chini yako.

Hoteli hii ni nzuri kwa kila hali, kuanzia mazingira hadi huduma za malazi na chakula. Ni aina ya hoteli ambayo unategemea kuiona katika miji mikubwa, si mji mdogo kama huu.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Nakubaliana na Prof. Ni hotel nzuri kwa kweli nimewahi kuwa hapa..

Mbele said...

Masista waliona mbali. Sasa Mbamba Bay imekuwa makao makuu ya wilaya ya Nyasa, nadhani mradi wao huu utapanda chati.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...