Tuesday, September 20, 2011

Nimekutana na Wapiga Debe Wangu Indianapolis

Nilikuwa Indianapolis kuhudhuria mkutano wa Africa Network, Septemba 16-18. Pamoja na mijadala kuhusu masuala mbali mbali, kuna mengi mengine yanayotokea katika mikutano ya aina hii. Nilikutana na wasomaji kadhaa wa kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, ambao ni wapiga debe wakubwa.

Hapa kushoto ni Profesa Tom Benson, mwanzilishi wa Africa Network, ambaye kabla ya hapo alikuwa mmoja wa waanzilishi wa Asia Network. Ni mzee maarufu katika ulimwengu wa taaluma na mashirika na taasisi za kimataifa. Yeye ni shabiki mkubwa wa kitabu hiki. Anakipenda na kukipigia debe.






Aliyesimama hapa kushoto akitoa mada ni Profesa John Tawiah Boateng wa Chuo cha Augustana. Anatoka Ghana. Ni shabiki mwingine mkubwa wa kitabu cha Africans and Americans. Katika programu yake ya kupeleka wanafunzi Ghana, wanafunzi wanakisoma kitabu hiki. Habari zake niliwahi kuzielezea hapa na hapa.






Aliyeweka mikono kidevuni, hapa kushoto, mbele kabisa, ni Profesa John Watkins anayefundisha hisabati katika Chuo cha Colorado. Ni mhamasishaji mkubwa wa masomo yahusuyo Afrika. Naye ni shabiki wa kitabu cha Africans and Americans. Wanafunzi wengi wanaoenda Afrika wamekisoma kitabu hiki kutokana na yeye kuwahamasisha.





Hapa kushoto anaonekana Profesa Edith Miguda wa Chuo cha St. Mary. Anatoka Kenya. Nilishawahi kumwona mara moja katika mkutano wa Africa Network. Katika mkutano wa Indianapolis aliniambia kitu ambacho sikujua, kwamba anakitumia kitabu cha Africans and Americans katika programu ya kupeleka wanafunzi Afrika. Nilifurahi kusikia hivyo.

Blogu yangu ni sehemu ninapojiwekea mambo yangu, iwe ni mawazo, hisia, kumbukumbu, au kingine chochote. Ni hiari yangu. Nimeona niwaenzi hao niliowataja. Imani yao juu ya kazi yangu inanifanya nijibidishe kufanya makubwa zaidi.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...