Tuesday, September 13, 2011

Mdau Kaleta Wadau Wengine


Kama nilivyowahi kuandika, tarehe 31 Agosti nilitembelewa na mdau Renatus Mgusii, ambaye anaonekana nami katika picha hapa kushoto. Ni mtu wa pekee kwangu, kwani ni msomaji makini wa vitabu vyangu. Ametumia hela zake nyingi kuvinunua na anapenda kuongelea yaliyomo. Pia ni mfuatiliaji wa blogu zangu. Ni wazi kuwa alivutiwa na mazungumzo yetu, hadi akaamua kuwaleta marafiki zake tuonane.


Wageni hao, ambao ni Mariana Ilieva na mumewe, aliwaleta tarehe 3 Septemba, pale Lion Hotel, Sinza. Mariana ni mkurugenzi wa Evin School of Management kwa upande wa Tanzania. Anajua lugha za ki-Bulgaria, ki-Rusi, ki-Swahili na ki-Ingereza. Mume wake, anayeonekana pichani, kulia kabisa, ni daktari m-Tanzania. Tuliongea mengi kuhusiana na taaluma na shughuli zetu sote wanne, na uwezekano na umuhimu wa kushirikiana. Ni jambo la kufurahisha kukutana na watu makini kama hao.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...