
Sikupata wasaa wa kufuatilia tangazo hili na kujua asili yake au kumfahamu mhusika. Kwa vile hapo ni madukani, nilihisi kuwa ni jina la duka liliopo hapa.
Kitu kidogo kama hiki ni changamoto kwa yeyote anayetafakari mambo. Suala la majina ya mahali mbali mbali ni suala linaloweza kutafitiwa, na sehemu mbali mbali duniani wataalam wanafanya utafiti wa namna hii.
Hapa kwetu Tanzania napo tunahitaji utafiti huo, tuweze kujua asili ya majina ya sehemu mbali mbali na hivyo kutunza kumbukumbu zake.

Majina mengine ya sehemu mbali mbali yanawataja watu maalum. Kwa mfano, kuna sehemu kule Msasani iitwayo "Kwa Mwalimu." Katika hospitali ya Muhimbili kuna wodi iitwayo Sewa Haji. Wangapi wanajua asili ya jina hili? Kuna sehemu pale Sinza iitwayo "Kwa Remmy." Nasikia kuna sehemu kule Manzese iitwayo "Kwa Mfuga Mbwa." Kama nilivyosema, haya ni masuala ya kutafitiwa.
No comments:
Post a Comment