Mmiliki ni Dada Neema, mjasiriamali anayeuza vitu mbali mbali, kuanzia vinyago, vikapu, na nguo za ki-Tanzania, hadi picha na postikadi za ki-Tanzania.
Nilionana naye hapa Bagamoyo mwaka jana, na ndipo alipofahamu habari za vitabu vyangu, akaamua awe anaviuza, kama wanavyofanya wajasiriamali wengine wawili watatu nchini Tanzania. Mimi si mfanyabiashara bali mwalimu na mwandishi. Ila niko tayari muda wote kuwawezesha wajasiriamali kuvipata vitabu vyangu. Namba ya simu ya duka la Dada Neema ni 0754 445 956.
No comments:
Post a Comment