
Nimevutiwa na huyu mtalii anayejisomea kitabu. Ninafahamu manufaa ya kusoma vitabu; navisoma kila siku. Nafahamu faida ya kuwa na vitabu, kwani ninavyo zaidi ya 3000.
Kama ninavyoandika mara kwa mara katika blogu hii na sehemu zingine, utamaduni wa kusoma vitabu uko sana miongoni mwa wa-Marekani. Ni kawaida kwa wa-Marekani kuwanunulia wenzao vitabu kama zawadi, kwa mfano kwenye nyakati muhimu kama Krismasi.
Wa-Marekani wanapokwenda nchi yoyote kama watalii, ni kawaida kwao kutafuta vitabu kuhusu nchi ile, wavisome kabla ya kusafiri, wakishafika kwenye nchi ile, au wakisharudi kwao. Ndio maana watalii hao hupenda sehemu zenye maduka ya vitabu.
Wa-Tanzania wangekuwa makini wangetambua na kuitumia fursa hiyo, kama nilivyoelezea katika kitabu cha CHANGAMOTO: Insha za Jamii. Lakini lazima nikubali kuwa kuweka mawazo na mawaidha katika kitabu haiisaidii jamii ambayo haina utamaduni wa kusoma vitabu.
No comments:
Post a Comment