
Tarehe 17 nilikuwa katika ziara ya sehemu kadhaa za mji wa Johanneburg. Sehemu moja tuliyotembelea inaitwa Newton, na hapo ndipo nilipopiga picha inayoonekana hapa. Nimekaa pembeni ya sanamu ya Kippie Moeketsi, mpiga saksofoni maarufu, aliyezaliwa mwaka 1925 na kufariki mwaka 1983.
Mwenyeji wetu aliyekuwa anatuongoza katika ziara hii alisema kuwa Kippie aliamua kubaki nchini Afrika Kusini pamoja na matatizo yote ya utawala wa makaburu.
Leo nimeangalia taarifa za mwanamuziki huyu mtandaoni, nikagundua kuwa huenda nilishasikia na kupendezwa sana na muziki wake. Hebu msikilize:
No comments:
Post a Comment