Saturday, June 8, 2013

Nimetoka Mbali na Kozi ya Hemingway

Kila siku, nawazia habari za mwandishi Ernest Hemingway. Kila siku nawawazia pia waandishi wengine, kutoka sehemu mbali mbali za dunia.

Hakuna siku inayopita nisisome angalau kurasa kadhaa za maandishi yao, au uchambuzi wa maandishi hayo. Kwa hilo, naweza kusema Hemingway ndiye anayetawala mawazo yangu kila siku.

Nilifanya utafiti na tafakari ya miaka kama sita hivi, kabla sijaunda kozi ya "Hemingway in East Africa." Kozi hii imeniwezesha kuzifahamu sehemu nyingi za Tanzania kaskazini, na  kufahamiana na watu wengi katika sehemu hizo.

Cha zaidi ni kuwa nimefahamiana na wanafunzi wengi wa ki-Marekani, waliokuja Tanzania kwenye kozi hiyo. Katika picha hapa kushoto, ambayo ilipigwa na Profesa Bill Davis wa chuo cha Colorado, ninaonekana nikitoa mhadhara juu ya Hemingway. Wanafunzi walikuwa kutoka chuo hicho. Huo ulikuwa ni mwaka 2008. Mara ya kwanza kufundisha kozi hiyo ilikuwa ni mwaka 2007, na wanafunzi walitoka chuo hicho hicho. Hapo ni katika viwanja vya chuo cha MSTCDC kilichopo eneo la Usa River, Arusha.

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

inapendaza kwa kweli....

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...