Saturday, June 1, 2013

Mama wa Mwanafunzi wa Kozi ya Hemingway Kanitembelea

Leo nimepata bahati ya kuonana na mama wa mwanafunzi mojawapo wa kozi ya Hemingway, ambayo niliifundisha Tanzania mwezi Januari. Mama huyu, mtoto wake, na mimi tunaonekana pichani hapa kushoto.

Mama kaja kutoka kwao Connecticut kujumuika na wahitimu wenzake wa chuo cha St. Olaf. Ni utaratibu wanaouita "reunion." Wanakuwepo chuoni kwa siku mbili tatu, wakiongelea masuala mbali mbali, pamoja na kujikumbusha miaka waliyosoma hapa. Laiti tungekuwa na utamaduni huu Tanzania.

Mama huyu alikuwa ameleta taarifa kabla, kupitia kwa mtoto wake, kwamba atapenda tuonane. Alisema ana nakala za kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, ambazo alitaka nizisaini. Ndivyo ilivyokuwa leo. Tulikutana, akanielezea jinsi mwanae alivyofaidi na kufurahia kozi ya Hemingway na fursa ya kuwepo Tanzania. Kisha ilisaini nakala zake tatu za hicho kitabu.

Kitabu hiki ni kati ya vile ambavyo wanafunzi walitakiwa kusoma kwa maandalizi ya safari ya Tanzania. Nimeshakutana na wazazi wengine ambao wamekisoma pia, na wanaponiona wanakizungumzia.

Mama huyu alishaniandikia barua kunishukuru kwa kufundisha kozi ya Hemingway, nami niliandika taarifa hii hapa. Maoni ya aina hii nimekuwa nikiyapata kutoka kwa wazazi wengine. Yananigusa sana na kunihamasisha nijibidishe zaidi katika kutekeleza wajibu wangu wa mwalimu na mlezi wa hao vijana. Mungu kanibariki kwa kunipa uwezo, nami nawajibika kutumia vipaji hivyo kwa faida ya walimwengu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...