Thursday, May 29, 2014

Duka Dogo Langoni pa Hifadhi ya Tarangire

Mwezi Januari, mwaka 2013, nilikuwa nazunguka maeneo ya kaskazini mwa Tanzania na wanafunzi 29 wa chuo cha St. Olaf. Tulikuwa katika kozi kuhusu safari za mwandishi Ernest Hemingway, tukisoma maandishi aliyoandika kuhusu sehemu hizo. Kati ya sehemu tulizotembelea ni hifadhi za Ngorongoro, Serengeti, Manyara, na Tarangire.

Kwenye sehemu ya kuingilia Tarangire, niliona duka dogo ambalo lilinivutia. Niliamua kupiga picha.



 


Kwa wale ambao wamefika Tarangire, hapa mahali ni karibu kabisa na Tarangire Safari Lodge. Ingawa nilishafika Tarangire mara mbili tatu miaka iliyotangulia, sikumbuki kama nililiona duka hili. Nilivutiwa na rangi mbali mbali za vitu vilivyokuwa vinauzwa humo. Nilijisikia kama vile naangalia kazi ya sanaa.

















Kwa wale ambao hawajafika, nimeona ni jambo jema kuwapa fununu kidogo kuhusu vitu ambavyo vinanivutia nchini mwetu.










No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...