Kwa macho, alionekana ndege mdogo. Lakini nilipompiga picha, nikiwa nimefungua "zoom" ya kamera, nimegundua kuwa alikuwa amebeba nyasi mdomoni. Bila shaka ni nyasi za kujengea kiota.
Nilivutiwa na jinsi ndege huyo alivyo na nidhamu. Alifanya kazi hiyo bila usimamizi au amri ya yeyote. Na aliifanya kwa uaminifu ina kujiamini. Laiti wanadamu wote tungekuwa na moyo wa aina hii.
No comments:
Post a Comment