Mkisimama hapo, mnauona mji wa Mto wa Mbu kule bondeni, na kwa mbali kule mbele mnaliona ziwa la Manyara.
Hata miaka iliyotangulia, wakati nasafiri na wanafunzi kutoka Chuo cha Colorado, tulifika mahali hapa. Mimi kama mwalimu naona ni muhimu kwa wanafunzi kufika sehemu hiyo na kuangalia sehemu hizi ambazo Hemingway alizielezea vizuri katika kitabu chake cha Green Hills of Africa. Inavutia kusoma maelezo ya Hemingway wakati mpo mahali hapa, anavyouelezea mji, mto unaopita hapo, duka la m-Hindu na uzuri wa Ziwa Manyara.
Nina imani kuwa sina haja ya kueleza kuwa anayeonekana hapo kushoto ni mimi.
No comments:
Post a Comment