Kwanza alifika ndugu Renatus Mgusii kutoka Segerea. Huyu tumefahamiana mtandaoni na ni msomaji wa maandishi yangu, kuanzia blogu hadi vitabu. Tuliongea mengi kuhusu masuala ya elimu, tofauti za tamaduni na athari zake katika dunia ya leo na mengine kadha wa kadha. Nimefurahi kukutana na mdau huyu, msomaji makini na mwenye uchungu na elimu.
Wednesday, August 31, 2011
Wadau Wawili Wamenitembelea
Leo hapa Sinza nimepata bahati ya kutembelewa na wadau wawili wa maandishi yangu.
Kwanza alifika ndugu Renatus Mgusii kutoka Segerea. Huyu tumefahamiana mtandaoni na ni msomaji wa maandishi yangu, kuanzia blogu hadi vitabu. Tuliongea mengi kuhusu masuala ya elimu, tofauti za tamaduni na athari zake katika dunia ya leo na mengine kadha wa kadha. Nimefurahi kukutana na mdau huyu, msomaji makini na mwenye uchungu na elimu.
Mdau wa pili alifika majira ya jioni. Huyu ni Gilbert Mahenge wa Msoga. Huyu niliwahi kuandika habari zake katika blogu hii, kwamba alikuwa mdau wa kwanza hapa Tanzania kununua na kusoma kitabu changu cha CHANGAMOTO. Niliguswa kumwona amefika na nakala yake. Tumeongea mengi kuhusu siasa, maendeleo na elimu. Alipiga simu Msoga nikapata fursa ya kumsalimia mkuu wa kijiji.
Kwanza alifika ndugu Renatus Mgusii kutoka Segerea. Huyu tumefahamiana mtandaoni na ni msomaji wa maandishi yangu, kuanzia blogu hadi vitabu. Tuliongea mengi kuhusu masuala ya elimu, tofauti za tamaduni na athari zake katika dunia ya leo na mengine kadha wa kadha. Nimefurahi kukutana na mdau huyu, msomaji makini na mwenye uchungu na elimu.
Tuesday, August 30, 2011
Safari ya Bagamoyo
Saturday, August 20, 2011
Matema Beach
Lakini nahisi kuwa siku itakuja ambapo wenye pesa watajichukulia sehemu hizi na kujenga uwigo hadi ziwani. Baada ya kuwekewa uzio, wananchi hawataweza kupita tena maeneo hayo. Hali hii nimeiona sehemu mbali mbali Tanzania, kama vile Ukerewe. Huu ni ubovu wa sera za serikali ya Tanzania ambao unanikera.
Friday, August 19, 2011
Mitaani Mbeya
Mbeya: Dobi Miwani Ameamia Sokoine
Napenda blogu yangu iwe bega kwa bega na wajasiriamali wadogo wadogo, katika harakati zao za kujitafutia chochote, kama nilivyogusia hapa.
Thursday, August 18, 2011
Niko Mbeya
Kwa vile ilikuwa ni usiku, sikuweza kuuona mji vizuri. Leo asubuhi nimeanza kutembelea maeneo ya mji, kama vile Mwanjelwa. Nategemea kupata fursa ya kuuona mji huu na pia sehemu zingine za mkoa wa Mbeya.
Wednesday, August 17, 2011
Leo Ninatimiza Miaka 60
Leo natimiza miaka sitini tangu kuzaliwa. Huu si umri mdogo, nami namshukuru Muumba kwa kunipa fursa ya kuwepo ulimwenguni kiasi hiki. Ninavyokumbuka maisha yangu, ninatamani kama ningekuwa nimefanya mengi na makubwa zaidi kuliko niliyofanya kwa manufaa ya wanadamu. Ninatamani kama ningekuwa nimejiepusha na mabaya, nikawa mtu bora wa kupigiwa mfano. Lakini haiwezekani tena kuirudisha miaka iliyopita. Bora niangalie mbele, nijaribu kufanya bidii zaidi, ingawa sijui nimebakiza miaka mingapi hapa duniani.
Friday, August 12, 2011
Kalenga Kwenye Makumbusho
Hapo ni mahala muhimu kwa kwenda kujifunza historia sio tu ya wa-Hehe bali ya Tanzania. Kwa mfano, katika makumbusho haya kuna kuna zana za mawe za kale zilizopatikana Isimila.
Idara inayohusika na hifadhi ya makumbusho hayo inafanya kazi nzuri katika mazingira magumu. Hata hivi, hakuna sababu yoyote kwa nini Tanzania isiweke kipaumbele katika kuipa idara hii kila msaada unaohitajika. Umma wa wa-Tanzania unapaswa pia kuamka ili utambue umuhimu wa makumbusho kama haya. Haipendezi, kwa mfano, kuona watu wanajichukulia viwanja na kujenga nyumba katika maeneo ambayo ni ya kihistoria. Wa-Tanzania tujiulize: je, iwapo ukuta mkuu wa China ungekuwa katika nchi yetu, tungekuwa tumeutunza kama wanavyofanya wa-China? Naogopa kuwa kutokana na elimu duni, watu wangeng'oa mawe ya ukuta huo na kujengea nyumba.
Wednesday, August 10, 2011
Msosi Iringa
Pichani naonekana na mwanafunzi Ryan Campbell tukiwa tunaudhibiti ugali na maini katika hoteli ya Wilolesi Hilltop, karibu na Kihesa. Ryan hakuushangaa ugali, kwani alishapambana nao Zambia alipokuwa na miaka 17.
(Picha imepigwa na Bailey Putney)
Tuesday, August 9, 2011
Nimeingia Iringa Jioni Hii
Tumesafiri na wadau wa programu ya Bega kwa Bega, ambao wanaishi Minnesota. Hii ni programu inayowashirikisha wa-Marekani na watu wa Iringa katika mipango mbali mbali ya maendeleo, kama vile elimu, afya, na maji safi. Ingawa mimi sikuwafahamu wadau tuliosafiri nao leo, wote wananifahamu. Wameniambia kuwa mwaandaaji na kiongozi wa safari yao, ambaye anaonekana pichani, wa pili kutoka kulia, aliwahimiza kusoma kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Ni faraja kwa mwandishi yeyote kujua kuwa watu wanasoma maandishi yake.
Tumefikia Iringa Lutheran Centre, na tutakuwa hapa wiki moja. Wadau wa hapa tunaweza kuonana katika siku hizo. Namba zangu za simu ni 0754 888 647 na 0717 413 073
Sunday, August 7, 2011
Mdau Kanitembelea
Aliniletea ujumbe kuwa anayapenda maandishi yangu akataka kuniona, kwani hatujapata kuonana. Alikodi teksi akanifuata. Yeye ni mtafiti makini mwenye nia thabiti ya kuchangia taaluma kwa maandishi. Tumeongea mengi, kuhusu utafiti na uandishi, pia umuhimu wa kuwahamasisha vijana kujiendeleza kielimu.
Friday, August 5, 2011
Mitaani Mbamba Bay

Mbamba Bay, ingawa mji mdogo sana, unavutia kwa utulivu wake na mazingira, ukiwa ufukweni mwa Ziwa linalomeremeta kwa maji yake maangavu, kama nilivyowahi kuandika hapa.




Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...