
Kama ni chama cha Kijamaa, kitanifurahisha, tofauti na CCM, chama ambacho kinahujumu ujamaa na mapinduzi kwa ujumla, kama yalivyoelezwa katika "Azimio la Arusha," "Mwongozo," na maandishi mengine.
Kuanzisha chama au kujumuika na wengine katika chama kwa misingi ya amani ni moja ya haki za binadamu. Na mimi nina haki ya kuwa nilivyo, raia ambaye si mwanachama wa chama cho chote cha siasa, haki ambayo inahujumiwa na katiba ya Tanzania iliyopo kwa kuwa inaniwekea vikwazo nikitaka kugombea uongozi katika siasa.
Pamoja na yote, ninapenda tu kusisitiza kuwa vyama vya siasa vijitegemee. Tutengue sheria ya kuvipa ruzuku, kama nilivyoandika katika blogu hii.
No comments:
Post a Comment