Thursday, July 2, 2015

Leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha Hemingway

Leo ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha mwandishi Ernest Hemingway. Alikufa tarehe 2 Julai, mwaka 1961, nyumbani mwake Ketchum, Idaho. Alikufa katika nyumba nayoonekana pichani ambayo ilipigwa na Jimmy Gildea wakati wa safari zake za kuandaa filamu ya Papa's Shadow.

Maelezo ya namna Hemingway alivyokufa yanapingana kidogo. Kila mtu anakiri kuwa alikufa kwa risasi ya bunduki. Karibu kila mtu anasema kuwa Hemingway alijiua kwa kujipiga risasi, akiwa peke yake ghorofa ya juu.

Lakini mke wake, Mary Welsh Hemingway, ambaye wakati wa tukio alikuwa katika nyumba hiyo kwa chini, alitoa tamko kuwa ilikuwa ni ajali:

Mr. Hemingway accidentally killed himself while cleaning a gun this morning at 7:30 A.M. No time has been set for the funeral services, which will be private.

Kila ninapowazia kifo cha Hemingway, nakumbuka jinsi alivyokuwa na mikosi ya ajali katika maisha yake. Ninavyowazia kuwa alijiua, nakumbuka misiba kadhaa ya watu kujiua katika ukoo wa Hemingway. Ninawazia pia kuwa mimi nimeishi miaka mingi kumzidi Hemingway, ambaye alizaliwa mwaka 1899 akafa mwaka 1962.

Ninajiuliza nimefanya nini katika miaka yangu yote hii, nikijifananisha na Hemingway, ambaye alikuwa mwandishi maarufu aliyeongoza njia kwa aina yake ya uandishi, akapata tuzo ya Nobel mwaka 1954.

Hemingway aliongelea kifo, tena na tena, katika maandishi yake. Kauli yake moja inayojulikana zaidi ni hii:

Every man's life ends the same way. It is only the details of how he lived and how he died that distinguish one man from another.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...