Wimbo huu hapa unatukumbusha tulikotoka, na mategemeo yetu miaka ya mwanzo ya Uhuru na hata baada ya "Azimio la Arusha." Tulipata Uhuru tukiwa na matumaini makubwa, na mojawapo alilieleza vizuri Mwalimu Nyerere:
Sisi tunataka kuwasha mwenge, na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, ili umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali palipo na chuki, na heshima palipojaa dharau.
Sunday, February 20, 2011
Monday, February 14, 2011
Mwanafunzi Wangu Kaniacha Hoi

Kabla ya kwenda Tanzania, alikuwa amechukua somo langu moja. Halafu, alipokuwa anaandaa safari ya Tanzania, tulikutana nikamweleza yale ninayowaelezea wa-Marekani kabla hawajaenda Afrika, kuhusu hali ya Tanzania, na hasa kuhusu tofauti za tamaduni kama nilivyozielezea katika kitabu cha Africans and Americans.
Alivyokuwa Tanzania, alikuwa akiangalia shughuli za madaktari katika hospitali moja mkoa wa Arusha. Kutokana na lengo lake la kuwa daktari, amejifunza mengi. Siku za mapumziko alisafiri hadi Dar es Salaam na Zanzibar, hifadhi za Ngorongoro, Serengeti na Lake Manyara. Pia alipanda Mlima Kilimanjaro.
Tulipomaliza maongezi, alinipa picha, bila mimi kutegemea, aliyopiga akiwa kileleni Mlima Kilimanjaro. Nimeguswa sana na zawadi hii. Raha moja kubwa ya ualimu ni kugusa mioyo, akili, na maisha ya wanafunzi. Nimevutiwa na ubunifu wa mwanafunzi huyu. Sikutegemea kuona jina langu linapepea juu ya Mlima Kilimanjaro. Labda ni changamoto, nijikongoje ili nami siku moja nikafike pale.
Sunday, February 13, 2011
Kitabu Kuhusu Mtume Muhammad

Kitabu hiki kinagusa na kuelimisha sana sio tu kuhusu historia ya u-Islam, bali pia kuhusu upekee wa Mtume Muhammad, kama Karen Armstrong anavyosema:
If we could view Muhammad as we do any other important historical figure we would surely consider him to be one of the greatest geniuses the world has known (uk.52). (Tafsiri yangu: Kama tungemtazama Muhammad kwa namna tunayowatazama watu wengine muhimu katika historia, ni wazi tungemtambua kama mmoja wa watu wenye vipaji vya ajabu kabisa ambao dunia imepata kuwafahamu).
Karen Armstrong ni maarufu kwa msimamo wake kuhusu u-Islam. Anaelezea sana historia ya zile anazoziita hisia potofu kuhusu u-Islam na zilivyoanza na kuenea. Lakini, pamoja na kutafiti na kuandika sana kuhusu u-Islam, Karen Armstrong ni mtafiti wa dini zingine pia, kama vile u-Kristu u-Juda, na u-Buddha. Ni mmoja wa watu wanaoongoza hapa duniani kwa umakini wa kuandika kuhusu dini.
Pamoja na kusoma kitabu cha Muhammad na kufuatilia maandishi mengine ya Karen Armstrong, na pamoja na kufuatilia mihadhara na mahojiano aliyotoa sehemu mbali mbali za dunia, nafuatilia pia maandishi na matamshi ya wengine kuhusu mchango wa Karen Armstrong. Nimebaini kuwa kuna malumbano kuhusu mchango wake, ambalo ni jambo la kutegemewa katika taaluma.
Kitabu cha Muhammad ni kizuri na muhimu sana. Nafurahi kukisoma, kwani kinanifungulia milango ya kuyafahamu maisha na mchango wa mtu ambaye ametoa mchango mkubwa sana duniani. Ni kitabu muhimu kwa yeyote mwenye nia ya kumwelewa Mtume Muhammad na kuuelewa u-Islam.
Karen Armstrong, ambaye alikuwa sista katika Kanisa Katoliki, ambalo ndilo dhehebu langu, anatuonyesha mfano mzuri, kwa kujibidisha katika kuzifahamu dini za wengine. Naamini kuwa iwapo sote tungefanya hivyo, kungekuwa na maelewano mazuri baina ya watu wa dini mbali mbali.
Thursday, February 10, 2011
Kitabu Kinapopigwa Marufuku
Kati ya mambo yanayosumbua sana akili yangu ni kitabu kupigwa marufuku. Sijui kama wewe unaafiki kupigwa marufuku kwa kitabu chochote.
Katika historia ya vitabu, ambayo ni karne nyingi, vitabu vingi vimepigwa marufuku sehemu mbali mbali za dunia, kwa sababu mbali mbali. Vingi vinaendelea kupigwa marufuku.
Tafakari matukio mawili ya kupigwa marufuku vitabu ambayo yametokea Tanzania. Kitabu kimoja ni Satanic Verses cha Salman Rushdie. Kuna watu waliona ni lazima kipigwe marufuku. Kingine ni Mwembechai Killings cha Dr. Hamza Njozi. Nacho kuna watu waliona ni lazima kipigwe marufuku.
Mtazamo wangu kuhusu suala hili nimeuelezea katika kitabu changu cha CHANGAMOTO, ambacho ni cha uchochezi. Labda nacho kitapigwa marufuku.
Katika historia ya vitabu, ambayo ni karne nyingi, vitabu vingi vimepigwa marufuku sehemu mbali mbali za dunia, kwa sababu mbali mbali. Vingi vinaendelea kupigwa marufuku.
Tafakari matukio mawili ya kupigwa marufuku vitabu ambayo yametokea Tanzania. Kitabu kimoja ni Satanic Verses cha Salman Rushdie. Kuna watu waliona ni lazima kipigwe marufuku. Kingine ni Mwembechai Killings cha Dr. Hamza Njozi. Nacho kuna watu waliona ni lazima kipigwe marufuku.
Mtazamo wangu kuhusu suala hili nimeuelezea katika kitabu changu cha CHANGAMOTO, ambacho ni cha uchochezi. Labda nacho kitapigwa marufuku.
Tuesday, February 8, 2011
Blogu Imenisaidia Darasani
Leo wakati muhula mpya unaanza hapa Chuoni St. Olaf, nimekutana na wanafunzi nitakaowafundisha somo la kuandika kwa ki-Ingereza. Kama kawaida, siku ya kwanza huwa ni ya kujitambulisha, kuelezea habari za somo, maana yake, falsafa na maadili yangu kama mwalimu, maana na mikakati ninayotumia katika kufundisha.
Katika kujitambulisha, huwa nawaeleza wanafunzi kuhusu nyumbani kwangu, shule nilizosoma, na nilivyoingia katika kazi ya ualimu, na imani yangu kuwa Mungu alitaka niwe mwalimu.
Leo wakati naanza kuelezea habari za nyumbani kwangu, nilikumbuka kuwa nilishaandika kwenye blogu. Basi, niliwasha kompyuta iliyomo darasani nikafungua blogu na wao wenyewe wakasoma kwenye skrini kubwa habari za Litembo.
Blogu imenisaidia kufikisha ujumbe wangu kwa ufanisi, kwani mbali ya maelezo kuna picha. Picha zinajieleza vizuri kuliko pengine hata maneno, jambo linalosisitizwa katika ule usemi kuwa picha ni sawa na maneno elfu. Niliwaambia kuwa nina picha nyingi za nyumbani kwangu na Tanzania kwa ujumla. Ni wazi kuwa ninazo fursa tele za kuendelea kuwajulisha walimwengu habari za kwetu.
Katika kujitambulisha, huwa nawaeleza wanafunzi kuhusu nyumbani kwangu, shule nilizosoma, na nilivyoingia katika kazi ya ualimu, na imani yangu kuwa Mungu alitaka niwe mwalimu.
Leo wakati naanza kuelezea habari za nyumbani kwangu, nilikumbuka kuwa nilishaandika kwenye blogu. Basi, niliwasha kompyuta iliyomo darasani nikafungua blogu na wao wenyewe wakasoma kwenye skrini kubwa habari za Litembo.
Blogu imenisaidia kufikisha ujumbe wangu kwa ufanisi, kwani mbali ya maelezo kuna picha. Picha zinajieleza vizuri kuliko pengine hata maneno, jambo linalosisitizwa katika ule usemi kuwa picha ni sawa na maneno elfu. Niliwaambia kuwa nina picha nyingi za nyumbani kwangu na Tanzania kwa ujumla. Ni wazi kuwa ninazo fursa tele za kuendelea kuwajulisha walimwengu habari za kwetu.
Thursday, February 3, 2011
Mji wa Moshi, Tanzania




Wednesday, February 2, 2011
Kauli ya Mufti Simba Kuhusu wa-Islam na Elimu

Nilikuwa njiani kuandika makala kuhusu suala la elimu katika historia ya u-Islam, ili kuiweka katika blogu hii. Baadhi ya mambo niliyopangia kusema ni kwamba u-Islam, tangu mwanzo, ulihimiza suala la elimu katika taaluma mbali mbali. Mtume Muhammad alisisitza suala hilo na waumini wakafuata kwa makini. Anayosema Mufti Simba ndio ukweli kwa mujibu wa dini ya ki-Islam.
Makala yangu inakuja. Kwa leo napenda tu kusema kuwa msisitizo wa Mufti Simba kuhusu elimu unatuhusu sisi wote, si wa-Islam peke yao. Ninaandika sana kuhusu suala hilo kwenye blogu na sehemu zingine, kama vile kitabu cha CHANGAMOTO, nikilalamika kuhusu uvivu uliokithiri miongoni mwa wa-Tanzania katika suala la elimu. Kwa hivi namwunga mkono na kumpongeza Mufti Simba kwa kusimama kidete kuongelea suala hilo. Yeye kama kiongozi wa wa-Islam amewataja wao, lakini ukweli ni kuwa nasaha zake zina manufaa kwa wa-Tanzania wote.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
-
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...