
Kitabu hiki kinaeleza kwa njia rahisi masuala mbali mbali ya kuzalisha fedha na matumizi ya fedha kwa namna ya kumsaidia mtu kuwa mwangalifu na kumfanya asonge mbele kimaisha. Kuna mawaidha mengi ya manufaa, hata katika masuala ya kuanzisha na kuendesha biashara na shughuli zingine za kujipatia kipato.
Kwa kuzingatia mabadiliko ya dunia, hasa katika tekinolojia ya mawasiliano, kitabu hiki kinatoa dokezo mbali mbali za kumwezesha mtu kutumia fursa zilizopo mtandaoni. Ingekuwa vijana wa Tanzania wana mazoea ya kusoma vitabu, wakawa wanasoma vitabu kama hiki, hata suala la ajira wangeliangalia kwa upeo tofauti, kwani ni aina ya kitabu kinachofungua milango ya ujasiriamali. Nina jambo moja tu la kushauri, kwamba ingefaa kitafsiriwe pia katika ki-Swahili.
Unaweza kumsikiliza Juanita akiongelea kitabu chake hapa. Kitabu hiki kinapatikana sehemu mbali mbali, kama ilivyoelezwa hapa.
No comments:
Post a Comment