Katika mhadhara wangu, uliodumu dakika 50, nilijikita katika kufafanua dhana mbali mbali zinazotumika katika utafiti na uchambuzi wa somo hili, ambazo chimbuko lake ni katika utafiti uliofanywa Ulaya, na jinsi dhana hizi zilivyopachikwa katika masimulizi ya sehemu zingine za dunia, kama vile Afrika. Nilihoji uhalali wa jambo hilo, ambalo tumelirithi na tunaliendeza.
Baada ya mhadhara wangu, tulikuwa na kipindi cha masuali, kilichodumu yapata dakika 40.
No comments:
Post a Comment